Bunge lavunjika Dodoma

Dar/Dodoma. Kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana usiku kilivunjika baada ya vurugu kutawala ukumbini humo.
Vurugu hizo zilianza saa 04:42 usiku hadi saa 04:49 usiku wakati Spika Anne Makinda alipolazimika kuahirisha Bunge hadi leo saa tatu asubuhi.
Chanzo cha vurugu ni kutokana na ugumu wa kutokukubaliana na azimio la tisa, lililolenga kumwajibisha moja kwa moja Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Azimio la PAC lilitaka Waziri Muhongo aadhibiwe kwa kufukuzwa kazi kutokana na tuhuma zilizokuwa zinazomkabili ikiwamo kulidanganya Bunge.
Hata hivyo, baadhi ya wabunge wengi wakiwa wa CCM walitaka waziri huyo asiadhibiwe... Soma zaidi
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Kenya yatoa uzoefu kwa Bunge la Katiba

Ujumbe maalum kutoka nchini Kenya umehutubia wajumbe wa Bunge la Katiba nchini Tanzania kuelezea uzoefu wao kuhusu mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya nchini Kenya ulivyofanyika.
Akizungumza na Wajumbe wa Bunge maalum la katiba, Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Kenya,Amos Wako ameainisha masuala ya msingi ya kuzingatia katika upatikanaji wa Katiba mpya ya Tanzania.
Bwana Wako ameeleza uzoefu wake wa upatikanaji wa katiba ikizingatiwa kuwa wakati mchakato wa kupata katiba mpya nchini Kenya alikuwa miongoni mwa watendaji wakuuu wa mchakato huo akiwa mwanasheria mkuu wa serikali. soma zaidi

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Chadema yampitisha Mathayo Torongey kupambana na Ridhwani Kikwete

Mgombea Ubunge wa Chalinze kwa tiketi ya Chadema, Mathayo Torongey akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana baada ya kutambulishwa. Picha na Michael Jamson Read More


[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la Kalenga ahutubia kwenye mvua, wananchi wavumilia

 Mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu Godfrey Mgimwa akiwa amebebwa juu na mmoja wa wanakijiji,mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wa kampeni wa uchaguzi mdogo wa jimbo hilo,uliofanyika katika kijiji cha Wenda kata ya Mseke-Iringa Vijijini,huku kukiwa na mvua kubwa ikinyesha,ambayo hata hivyo haikuzuia kufanyika kwa mkutano huo.Wananchi wa Kijiji hicho walionekana kuw ana shauku kubwa ya kutaka kumsikiliza Mgombea huyo bila kujali kulowana na mvua.Uchaguzi unatarajiwa kufanyika Machi 16.

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Kura ya Siri au wazi kaa la moto Bunge la Katiba

Na Daniel Mjema na Sharon Sauwa, Mwananchi


.......Habari kutoka katika kikao cha ndani cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), zilisema kutokana na mvutano huo, mjumbe mmoja, Chritopher Ole Sendeka, alijikuta akilia hadharani akitetea upigaji kura ya wazi.
Dodoma. Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, juzi na jana wamekuwa katika mtihani mgumu wa kufikia uamuzi wa pamoja kuhusu utaratibu wa upigaji kura, kati ya kura ya wazi na kura ya siri.

Habari kutoka katika kikao cha ndani cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), zilisema kutokana na mvutano huo, mjumbe mmoja, Chritopher Ole Sendeka, alijikuta akilia hadharani akitetea upigaji kura ya wazi.

Kikao hicho kilichofanyika juzi kati ya saa 2:00 na saa 5:30 usiku chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kilishuhudia mabishano makali kati ya wanaotaka kura ya siri dhidi ya wale wanaotaka kura ya wazi.

Habari hizo zilisema baada ya Pinda kufungua kikao hicho, alimkaribisha Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM, Shamsi Vuai Nahodha, ili atoe mrejesho wa kikao cha mashauriano.

Inaelezwa kuwa katika kikao hicho, Nahodha aliwaambia wajumbe kuwa kutokana na mazingira yaliyopo ndani na nje ya Bunge kwa upande mmoja na wananchi kwa upande mwingine, kura ya siri haiepukiki.

“Kilio cha Ole Sendeka kwenye party cocas kikao cha chama (party cocus) juzi usiku kilitokana na kauli ya Nahodha kwamba kura ya siri haiepukiki,” alidokeza mbunge mmoja wa CCM aliyehudhuria kikao hicho cha faragha.

Mbunge huyo alilidokeza gazeti hili kuwa ndani ya kikao kulikuwa na mabishano makali baada ya kauli ya Nahodha, huku baadhi ya wabunge wakisema wananchi wamechoshwa na msimamo wa CCM.

Ni kutokana na mabishano hayo ndipo Ole Sendeka aliposimama akipinga mapendekezo yaliyotaka CCM kulegeza msimamo na kuridhia kura ya siri na wakati alipokuwa akizungumza alipobubujikwa na machozi.

Huku akilia katika kikao hicho, inadaiwa Ole Sendeka akisema kwamba kukubali kura ya siri ni kuitosa CCM na msimamo wake wa kutaka muundo wa Serikali mbili.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho, zilidai kuwa Ole Sendeka alienda mbali zaidi na kusema endapo Pinda ataridhia kura hiyo ya siri, basi yeye (Pinda) na viongozi waandamizi wa CCM waliohudhuria watawajibishwa na CCM.

Kutokana na mtafaruku huo, kikao hicho kilishindwa kufikia mwafaka na kuahirishwa hadi jana saa 5:00 asubuhi ambapo hoja ya ama kura ya siri au ya wazi, iliendelea kuwagawa wabunge katika makundi mawili.

Wakati akifungua kikao cha jana, Pinda alisema kutokana na yaliyotokea katika kikao chao cha juzi usiku na baada ya kutafakari kwa mapana yake, chama kimeamua kibakie na msimamo wake wa kura ya wazi.

“Kutokana na yaliyojitokeza jana (juzi) na hasa ukiona mtu mzima analia, tumetafakari tumeona tubaki na msimamo wa kura ya wazi,” alisema mmoja wa wabunge akimkariri Waziri Mkuu Pinda.
Kwa mujibu wa mbunge huyo, katika kikao hicho ilielezwa kuwa kukubali upigaji kura wa siri ni kuiua CCM kwa sababu wajumbe wengi wa Bunge Maalumu la Katiba, watapitisha muundo wa Serikali tatu badala ya mbili.
Katika hatua nyingine, baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wamehoji kitendo cha Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho kuhudhuria kikao cha ndani cha wabunge wa CCM.
“Kificho ni mwenyekiti wa Bunge lenye makundi tofauti, sasa anapoingia kwenye kikao cha wabunge wa CCM kinachoweka mikakati ya kupingana na makundi mengine anatoa picha gani?” alihoji mbunge mmoja.
Taarifa za Kificho kuhudhuria kikao hicho cha jana cha CCM zilionekana kuwakera wajumbe wengine wa Bunge hilo, wanaotokana na vyama vya upinzani na wale wanaotoka katika kundi la wajumbe 201.
“Bado tunatafakari tuchukue uamuzi gani, lakini tukiona vipi, tutasusia kikao cha leo (jana) jioni, nyie njooni ndani lolote linaweza kutokea,” alidokeza mjumbe huyo anayetoka katika kundi la vyama vya hiari.
Kura ya siri, wazi yawekwa kiporo
Hata hivyo, jana mara baada ya Kificho kuanza kikao cha semina saa 10:40 alasiri badala ya saa 9:00 alasiri alisema semina hiyo imechelewa kuanza kwa sababu ya masuala muhimu.
Kificho aliwaambia wajumbe kuwa kamati ya mashauriano ilikuwa imemshauri kanuni ya 37 na 38 zinazohusu kura ya siri viwekwe kiporo kutokana na kutopatikana kwa mwafaka.
“Kamati imenishauri bado tuache kanuni ya 37 na 38 ili kamati ya mashauriano iendelee kunishauri vizuri zaidi ili baadaye tuje tuwaambie kamati ya kanuni iziandike vipi,” alisema.
Kutokana na ombi hilo, wajumbe waliafiki waendelee kupitia kanuni ya 32 hadi 36 na 39 hadi 43 ambavyo havina mvutano.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

OXFAM YAIVURGA LOLIONDO

*Yazifadhili asasi kuvuruga amani Loliondo
*Yazichotea mamilioni kufanikisha vurugu

Shirika la Misaada la Kimataifa la Oxfam limejiingiza kwenye ufadhili wa vikundi na asasi za kiraia, zinazozua na kuchochea mgogoro kati ya Serikali na wafugaji wa jamii ya Kimaasai katika Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha.
Kujiingiza kwa Oxfam ni juhudi za asasi za Tanzania zilizo na baadhi ya raia wa kigeni, kuhakikisha kuwa Loliondo haitawaliki. Pia ni mwendelezo baada ya kukwama kwa baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya Ulaya ambao mwaka jana walijiingiza huko kinyemela hata bila kuitaarifu Serikali ya Mkoa wa Arusha.

Habari za uhakika zilizopatikana kutoka Arusha zimesema kwamba shirika hilo limetoa mamilioni ya shilingi zilizowezesha baadhi ya asasi hizo kukutana mjini Arusha wiki iliyopita. Fedha hizo, pamoja na kuwawezesha viongozi na wanachama wa asasi hizo, zinatumika pia kulipia matangazo na propaganda katika vyombo vya habari.

Asasi zilizo katika mkakati huo ni mtandao wa wanaharakati wa haki za binadamu (FEMA CT), mtandao wa mashirika yanayotetea haki za wafugaji, wawindaji na wachuma matunda nchini (PINGO’s Forum), mtandao wa utetezi wa masuala ya ardhi (TALA), na shirika lisilo la kiserikali lililopo Ngorongoro (NGONET).

Asasi hizo kwa mara ya kwanza kwenye tamko lake, kwa vyombo vya habari mwishoni mwa wiki, zimetamka wazi kuunga mkono harakati za kuichafua Tanzania zinazoendeshwa kwenye mtandao.

“Kutokana na hayo, sisi mashirika yanayojishughulisha na utetezi wa haki za binadamu nchini Tanzania, tunaunga mkono kampeni za mtandao wa kimataifa wa Avaaz,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Kufanyika kwa mkutano wa pamoja wa asasi hizo kumekuja baada ya hivi karibuni Rais wa Oxfam Ireland, Monica Gorman, na viongozi wengine wa shirika hilo kuzuru Ngorongoro bila kuwataarifu viongozi wa Serikali ngazi ya mkoa.

Akiwa Loliondo, Gorman alijaribu kuibua tatizo “lisilokuwapo” na kutaka wananchi wanaoishi hapo wasibughudhiwe. Kimsingi anapinga kusudio la Serikali ya kuandaa Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi katika vijiji vya Loliondo. Mpango huo umelenga kuainisha maeneo ya malisho ya mifugo, maeneo ya uhifadhi wanyamapori, maeneo ya kilimo, na shughuli nyingine za kijamii.

Akiwa katika Kijiji cha Arash kilicho karibu na Loliondo, aliwataka wanavijiji wawe makini katika kuingia mikataba na kampuni kwa maelezo kwamba watapoteza ardhi yao.

Wengine waliokuwa kwenye msafara huo ni Mkurugenzi Mkuu wa Oxfam, Jim Clarken; Mwenyekiti wa Kamati ya Uhusiano wa Mambo ya Nje wa Bunge la Ireland, Jim Wells, na Pat Breen, ambaye ni Mbunge.

Mwenyejiti wa Arash, Kiaro Orminis, aliueleza ujumbe huo kwamba kuna matatizo ya ardhi katika eneo hilo, hasa unaohusisha Kijiji cha Malambo na kampuni ya uwindaji wa kitalii ya Ortello Business Corporation (OBC).

Kwa muda sasa, mgogoro katika eneo la Loliondo ulikuwa umetulia hasa baada ya wananchi kuelimishwa juu ya umuhimu wa kupanga matumizi bora ya ardhi.

Utulivu huo umekuwa ukiathiri mapato ya asasi zinazojitanabaisha kuwa zinawatetea wafugaji, ilhali zikiwa hazifanyi juhudi za kutosha katika kuwasaidia wananchi hao.

Kampeni ya hivi karibuni ilipamba moto kwenye mtandao wa Avaaz, ikidai kwamba Serikali ilikuwa mbioni kuwahamisha wafugaji wa Kimaasai kutoka Serengeti. Taarifa hiyo ilipingwa vikali na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii.

Taarifa ya Serikali ya Agosti 15
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Khamis Sued Kagasheki, amekanusha uvumi unaosambazwa na shirika moja kupitia mtandao wake wa AVAAZ.org kuwa Watanzania wa jamii ya Kimaasai wapatao 48,000 watahamishwa kutoka eneo lao (la Serengeti), kupisha wafalme kutoka Mashariki ya Kati ili walitumie eneo hilo kwa uwindaji wa simba na chui.

Taarifa hiyo iliyosambazwa na mtandao huo imewataka watu kutoka duniani kote kujiorodhesha ili wafikie angalau 150,000, ili kumshinikiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuacha kusaini mkataba utakaofanya uhamisho huo utekelezwe.

Waziri Kagasheki amesisitiza kuwa uvumi huo si wakweli na hauna msingi wowote kutokana na sababu zifuatazo:

Kwanza, hatua kama hii haiwezi kuchukuliwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Hifadhi ya Serengeti maana hakuna watu wanoishi ndani ya hifadhi hiyo. Pia kitendo hicho hakijapangwa kufanyika katika Wilaya ya Serengeti iliyoko mkoani Mara.

Pili, hata kama taarifa hiyo ilimaanisha Wilaya ya Serengeti mkoani Mara bado si yakweli maana wilaya hiyo haina idadi ya Wamaasai wanaofikia jumla ya 48,000.

Tatu, ndani ya ya Hifadhi ya Serengeti hakuna eneo lolote lililotengwa kwa ajili ya wafalme wa Mashariki ya Kati, ili waweze kulitumia kwa uwindaji wa simba na chui.

Nne, habari hizo si za kweli maana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hahusiki kabisa na ugawaji wa vitalu vya uwindaji popote pale nchini. Hii ni kazi ya Wizara ya Maliasili na Utalii, na Wizara haijafanya hivyo katika eneo tajwa.

Pamoja na ufafanuzi huo, Waziri Kagasheki amewaasa watu waliojiorodhesha na wanaotarajia kujiorodhesha, kuwa wamepotoshwa, hivyo wanatakiwa wasisaini kubariki kitu ambacho hawakijui wala hakipo.

CHANZO - JAMHURI
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

YANGA NA SIMBA WAKABIDHIWA VIFAA NA KILIMANJARO

Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu (kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ (kulia), wakionesha baadhi ya vifaa vya michezo  walivyokabidhiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ambao ndio wadhamini wakuu wa klabu hizo. Wa pili kushoto ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe na Mkurugenzi wa Mashindano, Saad Kawemba. Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jijini Dar es Salaam
 
Na Clezencia Tryphone
KLABU kongwe nchini za Simba na Yanga, zimekabidhiwa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya sh milioni 34 kila moja kutoka kwa mdhamini wao mkuu, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager.
Akikabidhi vifaa hivyo katika Ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jijini Dar es Salaam, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe, alisema, kukabidhi vifaa hivyo ni moja ya sehemu katika mkataba baina yao na klabu hizo.
Kavishe alisema lengo kubwa la kudhamini timu hizo ni kutokana na historia kubwa ya klabu hizo, pamoja na kuleta ushindani wenye burudani kwa Watanzania, ambao ni wadau wakubwa wa kunywa kinywaji hicho.
“Sisi tunafanya kazi vema na klabu hizi, tunajisikia faraja kubwa kutokana na timu hizi kuwa na historia kubwa hapa nchini na ushindani mkubwa katika soka na huu ni udhamini wa nusu msimu peke yake,” alisema Kavishe.
Alivitaja vifaa hivyo walivyotolewa kuwa ni jezi, bukta, soksi, viatu, bips, nguo za kusafiria, vikinga ugoko na mifuko.
Katika hatua nyingine, Kavishe alisema, kuhusu mabasi ya timu hizo, wako katika hatua za mwisho kuyakabidhi kwa wahusika, kwani tayari yamewasili hapa nchini, ambapo kuna mambo kadhaa wanayakamilisha.
Akizungumza kwa niaba ya klabu ya Simba, Makamu Mwenyekiti, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, aliwashukuru wadhamini hao kwa moyo walionao, huku akiwaahidi kuhakikisha wanafanya vema na kushinda ili kuonesha umuhimu wa vifaa ambavyo wamewapa.
“Nawashukuru TBL kwa kutudhamini na kuona umuhimu kwa sisi Simba bila ya kupepesa macho na ndiyo maana hata sisi tutapigana kufa na kupona ili kuhakikisha tunavitendea haki vifaa hivi,” alisema Kaburu.
Kwa upande wa Yanga, Ofisa Habari wake, Louis Sendeu, naye aliishukuru TBL, huku akiwaomba kutoishia kwa Simba na Yanga, bali waziangalie na timu nyingine.
“Tunawashukuru sana ila msiishie kwa Yanga na Simba tu, mziangalie na klabu nyingine ambazo zinasuasua,” alisema Sendeu.
CHANZO : Francis Dande
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

DK MARY NAGU ANG'OKA NEC HANANG'

MBIO za uchaguzi ndani ya CCM zimefikia patamu, baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Dk Mary Nagu kuenguliwa kugombea nafasi ya Ujumbe wa Nec kupitia Wilaya ya Hanang', huku Mke wa Rais, Salma Kikwete akiwa mgombea pekee wa nafasi hiyo Lindi Mjini.

Mkoani Dar es Salaam, mbio hizo zimeonekana kuwaweka pabaya Mwenyekiti wa UWT wa mkoa huo Zarina Madabida na Katibu wake, Tatu Maliaga baada ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa, John Guninita kueleza kuwa viongozi hao watafikishwa kwenye kamati ya maadili kueleza kwa nini wamesitisha uchaguzi wilayani Kinondoni.

Habari kutoka Hanang' zimeeleza kuwa Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya hiyo imemwengua Dk Nagu na kuwabakiza wagombe wawili, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye na Leonsi Marmo.

Taarifa kutoka kwenye kikao hicho kilichofanyika juzi katika Ofisi ya CCM ya wilaya hiyo na kuhudhuriwa na wajumbe 12 zimeeleza kuwa Dk Nagu ameenguliwa kutokana na maelezo kuwa kanuni hazimruhusu kugombea.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa kanuni iliyomwondoa Dk Nagu kwenye kinyang’anyiro hicho ni ile inayowataka viongozi wenye kazi za kila siku; ubunge na uwaziri kutogombea.

Imeelezwa kuwa jitihada za wajumbe watano waliojipambanua katika kikao hicho kumtetea Dk Nagu ziligonga mwamba, baada ya wenzao saba kuunga mkono uamuzi huo.

“Kikao kilikuwa kizito, lakini tulitazama zaidi kanuni, sifa za wagombea na uwezo wa wagombea hasa katika nafasi hii nyeti ya Nec kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015,” alisema mmoja wa wajumbe wa kikao hicho.
Alisema mapendekezo ya kikao hicho, tayari yamefikishwa ngazi ya CCM mkoa kwa uamuzi zaidi na baadaye yatafikishwa Kamati Kuu (CC) ya CCM.

“Sisi tumemaliza kazi yetu, tunaamini kuwa tumetenda haki kwa manufaa ya chama chetu Wilaya ya Hanang’,” alisema kiongozi huyo.

Hata hivyo, mjumbe mwingine wa kikao hicho alisema, mgawo wa mkopo wa matrekta ambao umekuwa ukiendelea Hanang’ umechangia kumwengua waziri huyo.

“Hapa kuna mambo mengi, nadhani hao waliokuwa na taarifa hizi, wameshindwa kueleza zaidi. Kuna mambo ya chinichini hasa baada ya baadhi ya viongozi kutounga mkono uamuzi wa Waziri Nagu kusaidia baadhi ya wanaCCM wakiwamo viongozi kukopeshwa matrekta,” alisema mjumbe huyo.

Kiongozi mmoja wa CCM Wilaya ya Hanang’ ambaye hakutaka jina lake litajwe, alikiri kufanyika kwa kikao hicho na kueleza kuwa tatizo la Dk Nagu ni kutoombewa kibali na kamati ya siasa wilaya au mkoa kama kanuni zinavyotaka.
Alieleza kuwa kanuni za CCM zinataka viongozi wenye majukumu ya kila siku kuombewa kibali kwanza na Kamati ya Siasa ya Wilaya au Mkoa kabla ya kugombea jambo ambalo halikufanyika kwa Dk Nagu.

“Hadi kikao hicho kinafanyika, Dk Nagu alikuwa hajaombewa kibali hicho na hili limetokana na migogoro ya kisiasa iliyoko wilayani Hanang’,” alisema.

Alipoulizwa kuhusu hilo, Katibu wa CCM Wilaya ya Hanang’, Allan Kingazi alisema: “Ni kweli kikao kilifanyika, lakini mapendekezo yetu ni siri na hao waliokuambia wamekiuka kanuni. Sisi baada ya kumaliza kikao chetu, mapendekezo yetu tumeyapeleka ngazi ya mkoa ambako pia yataendelea kuwa siri hadi majina yatakapotangazwa rasmi,” alisema.

Uamuzi wa Dk Nagu kuamua kugombea NEC kupambana na Sumaye ambaye ndiye alimwachia jimbo hilo, ulitabiriwa kuibua mgawanyiko mkubwa ndani ya wana CCM wa Hanang’.
Jitihada za gazeti hili kumpata Dk Nagu kuzungumzia uamuzi huo zilishindikana baada ya simu yake ya mkononi kuita muda mrefu bila kupokewa.

Kuenguliwa kwa Dk Nagu kunatokana na sababu za kuwa na kazi za muda wote kumeibua hofu kuhusu hatima ya viongozi wengine waliochukua fomu ambao kwa mujibu wa kanuni iliyomwondoa Dk Nagu nao hawakupaswa kugombea.
Hao ni pamoja na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Abdallah Kigoda, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk Emmanuel Nchimbi.

Wengine ni Wabunge Deo Filikunjombe (Ludewa), Mussa Azzan Zungu (Ilala), Dk Hamis Kigwangalla (Nzega) na Andrew Chenge (Bariadi Magharibi).

Salma akosa mpinzani Lindi
Katika hatua nyingine Mke wa Rais, Salma Kikwete amerudisha fomu ya kuwania ujumbe wa Nec Taifa kupitia Wilaya ya Lindi Mjini.

Katibu wa CCM Wilaya ya Lindi Mjini Mohamed Kateva, alisema jana kwamba Salma ni mgombea pekee aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo katika wilaya yake.

Kateva alisema mwisho wa kurudisha fomu ilikuwa Agosti 28, mwaka huu na mpaka tarehe hiyo hakukuwa na mtu mwingine aliyekuwa amejitokeza kuwania nafasi hiyo.

Madabida kiti moto

Katika Mkoa wa Dar es Salaam, Madabiba na Maliaga watahojiwa kwa kukiuka uamuzi ya Halmashauri Kuu ya Mkoa.
Viongozi hao wanadaiwa kusimamisha uchaguzi wa UWT Wilaya ya Kinondoni ambao ulipangwa kufanyika Agosti 31, mwaka huu.
Guninita alisema jana kuwa kikao hicho cha Nec mkoa kiliagiza uchaguzi wa jumuiya zote ufanyike kuanzia Agosti 31 hadi Septemba 2, mwaka huu lakini UWT Wilaya ya Kinondoni haikufanya uchaguzi huo.
Alisema katika kikao chake cha Agosti 29, mwaka huu Nec Mkoa kilipitisha wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika wilaya zote tatu na kuagiza uchaguzi ufanyike.
“Mwenyekiti wa UWT na katibu wake kwa sababu zao binafsi walisimamisha uchaguzi na kwa mujibu wa katiba yetu hili ni kosa,” alisema Guninita.
Alipotakiwa kuzungumzia madai hayo Madabida alisema: “Nipo kikaoni. Lakini ndani ya chama chetu cha CCM hakuna mtu anayeweza kuusimamisha uchaguzi peke yake.”
Habari hii imeandikwa na Nora Damian, Dar; Mussa Juma, Hanang' na Mwanja Ibadi, Lindi.

 CHANZO - MWANANCHI
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MAFUTA BEI JUU

Mwandishi Wetu   
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli nchini ambapo bei ya  petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepanda.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo jana bei mpya zitaanza kutumika kuanzia leo.

"Sambamba na kupanda kwa gharama halisi za uagizaji wa mafuta kutoka kwenye Soko la Dunia, bei za jumla na rejareja kwa mafuta aina zote zimebadilika ikilinganishwa na taarifa iliyopita ya Agosti 1, 2012," ilieleza taarifa hiyo.

Kaguo katika taarifa hiyo alieleza kuwa bei za rejareja kwa Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka,  ambapo Petroli imepanda kwa Sh 291 kwa lita sawa na asilimia 14.50; Dizeli Sh 199 kwa lita sawa na asilimia 10.26; na Mafuta ya Taa Sh 67 kwa sawa na asilimia 3.47.

"Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya mawili zimebadilika kama ifuatavyo: Petroli imeongezeka  kwa Sh 291.54 kwa lita sawa na asilimia 15.07; Dizeli Sh 199.57 kwa lita sawa na asilimia 10.68 na mafuta ya taa kwa Sh 67.29 kwa lita sawa na asilimia 3.63," aliseleza katika taarifa hiyo.

Alisema kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani ilimradi bei hizo ziko chini ya bei kikomo kama ilivyokokotolewa na kanuni mpya iliyopitishwa na Ewura  na kuchapwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 454 la Desemba 23, 2011.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

SIRI NZITO ZAANZA KUJITOKEZA KIFO CHA MWANGOSI

POLISI WALIOTEKELEZA OPERESHENI WADAIWA KUSAFIRISHWA KUTOKA MIKOA MINGINE, WAANDISHI WA HABARI IRINGA WASUSIA MKUTANO WA DCI MANUMBA
 
INADAIWA kwamba askari waliokuwa katika operesheni ya kuzuia mkutano wa Chadema katika eneo la Nyololo wilayani Mufindi, Iringa na ambayo ilisababisha kifo cha Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi walitolewa katika mikoa ya Dodoma, Morogoro na Mbeya.


Tayari tukio hilo limeibua mjadala mzito kiasi cha kumfanya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi kuunda tume huru kubaini chanzo cha tukio hilo. Marehemu Mwangosi alizikwa juzi nyumbani kwao Tukuyu, mkoani Mbeya.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili jana zilisema kuwa polisi hao kutoka mikoa hiyo mitatu wakiwa wamesheheni vifaa mbalimbali likiwamo gari la maji ya kuwasha, walisafiri siku moja kabla ya mkutano huo wa Chadema na baadaye kuzuka vurugu zilizosababisha kifo hicho.
Marehemu Mwangosi aliuawa kwa mlipuko unaodhaniwa kuwa ni wa bomu ambao ulisambaratisha vibaya sehemu kubwa ya mwili wake.


Chanzo cha habari kutoka mkoani Dodoma kilisema: “Hapa kwetu kuna askari 10 na tunawafahamu kwa majina. Waliondoka hapa siku moja kabla ya tukio hilo wakiwa na gari la washawasha.”
Chanzo hicho kilisema kwamba awali, hawakuwa wakifahamu kama baadhi ya wenzao walichukuliwa na kupelekwa Iringa. “Tulikuja kuona kwenye gazeti picha na tulipofuatilia tukaelezwa kuwa ni kweli Dodoma ilitoa askari kwenda Iringa.”


Askari mwingine aliyekuwa katika operesheni hiyo ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sababu za kitaaluma, alikiri kuwa hadi jana baadhi yao walikuwa bado wako Iringa na kwamba walikwenda kwa agizo la wakubwa wake wa kazi.
“Sisi ni Watanzania, lakini tumelazimika kuyafanya hayo kwa sababu ya mkate (malipo). Kwa kweli haikuwa haki, kuwatoa askari na silaha kutoka mikoa mitatu kana kwamba wanakwenda kupigana vita!”


Alidokeza kwamba, askari wote waliotoka Dodoma walikuwa njiani kurudi mkoani humo, jana lakini gari la maji ya kuwasha liliendelea kubaki huko Iringa likiwa na dereva wake na askari mmoja mwenye cheo cha inspekta. Askari huyo alisema kwamba gari hilo lililazimika kubaki kutokana na hitilafu.

“Wengine wamerudi lakini, kuna wengine wenye gari la kuwasha bado walikuwa Iringa, gari lao limepata hitilafu kidogo,” kilisema chanzo hicho kutoka mjini Dodoma.

Mmoja wa askari hao alidaiwa kwamba hiyo inaweza kuwa moja ya sababu ya askari hao kumshambulia marehemu Mwangosi wakati mwenzao anayemfahamu akijaribu kuwazuia. "Hii inaonyesha kuwa askari hao waliompiga walikuwa hawamjui na huyu aliyekuwa akiwazuia, alimjua.”

Makamanda watupiana mpira

Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen hakukubali wala kukanusha na badala yake alisema: “Mambo yote hayo yanatakiwa kujibiwa na Kamanda wa Iringa.”
Aidha, alisema sakata la kifo cha mwandishi huyo kwa sasa liko katika vyombo vya uchunguzi hivyo asingekuwa tayari kulizungumzia.


“Siwezi kusema kama askari wangu walikwenda huko au hawakwenda, isipokuwa ninachoweza kusema ni kwamba suala hilo lipo katika vyombo husika hivyo waachiwe wao au Kamanda wa Iringa ndiye mwenye majibu.”
Alipotajiwa jina la mmoja wa askari aliyeonekana katika picha za video na magazeti za tukio hilo kwamba anatokea katika moja ya vituo vyake, kamanda huyo alisema: “Mimi yakitokea Dodoma nitazungumza wala siyo mtu mwingine kwa hiyo, mambo ya Iringa siwezi kuyazungumza na kama tutaanza kila Kamanda kuzungumza jambo hilo hamuoni kuwa itakuwa ni kama vurugu?”


Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda alipopigiwa simu yake iliita tu bila kupokewa.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile alisema kwa kuwa tukio hilo limefanywa na polisi, mambo mengi yatazungumzwa lakini akasisitiza kwamba hajapeleka askari Iringa.

Alisema hakukuwa na agizo kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi wala ombi kutoka Polisi Iringa kutaka askari wa kuongeza nguvu... “Taarifa hizo ni za uzushi kwani hazina ukweli wowote.”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani alikanusha pia kuwapeleka askari wake Iringa akisema: “Hizo taarifa siyo za kweli. Hakuna askari yeyote aliyekwenda Iringa wakati wa vurugu zile.”


Mkutano wa DCI wavunjika

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba hakutaka kuzungumzia suala hilo akisema: “Hayo yote yameundiwa tume ngoja tuiachie ifanye kazi yake.”
Awali, DCI Manumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari mkoani Iringa, ambao hata hivyo, ulivunjika baada ya kutokea kutoelewana baina yao.


Manumba alitaka kueleza ripoti ya uchunguzi wa kifo cha Mwangosi, lakini waandishi hao walikataa kumsikiliza wakisema hawauamini uchunguzi huo kwa kuwa ulifanywa na polisi peke yao.

Kabla Manumba, hajaanza kuzungumza, Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Iringa (IPC), Frank Leonard alisema kutokana na msimamo wa waandishi wa habari wa mkoa huo hakutakuwa na uhusiano wa kikazi na polisi hadi pale tume zilizoundwa kuchunguza kifo hicho zitakapotoa taarifa sahihi juu ya mauaji hayo.

“Msimamo wetu ni kusitisha uhusiano wa kikazi baina yetu na jeshi la polisi hususan Mkoa wa Iringa, tumekuja hapa kwa sababu DCI umetuita na kama unataka kutupa taarifa ya kifo cha ndugu yetu basi waambie hao maofisa wa jeshi wa Iringa watoke nje,” alisema Leonard.

Akijibu madai hayo Manumba alisema: “Nia yangu ni kutoa taarifa ya uchunguzi wa kifo cha Mwangosi, ndiyo maana niliwasiliana na mwenzenu ili tuweze kuzungumza, Polisi Iringa wataendelea kuwepo na waandishi wa habari mtaendelea kuwepo, matukio kama haya yapo na yataendelea kuwepo.”
Licha ya maelezo hayo, hakuna mwafaka uliofikiwa na mkutano huo ukavunjika.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili baadaye, DCI Manumba alisema: "Ni vyema wao wangenisikiliza kujua ninataka kuwaambia nini. Lakini, kwa kuwa kuna mkanganyiko, nimeona ni vyema jambo hili lisubiri tume ndipo watakuja kulizungumza.”


Waikataa Tume ya Nchimbi
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeiponda tume ya Dk Nchimbi kikieleza kuwa imeundwa ili kurudisha uhusiano kati ya Polisi na waandishi wa habari na si kutafuta chanzo cha tatizo.


Juzi, Dk Nchimbi alitangaza kamati ya kuchunguza mauaji hayo inayoongozwa na Jaji Mstaafu, Steven Ihema na wajumbe, Mwakilishi wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga, Mwakilishi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Pili Mtambalike, Mtaalamu wa milipuko kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kanali Wema Wapo na Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Isaya Mngulu.

Mkurugenzi wa Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu alisema Dar es Salaam jana kwamba: “Hii si tume ya kuchunguza mauaji, bali ina lengo la kurudisha uhusiano mzuri kati ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari ili kuwasahaulisha wananchi kwa sababu imeundwa na waziri ambaye naye anatakiwa kuhojiwa.” “Tunamwomba Rais Jakaya Kikwete ateue tume kama anavyoelekezwa na Sheria ya Tume za Uchunguzi ya mwaka 1992, ambayo inaruhusu kumhoji yeyote kasoro yeye Rais.”

Lissu alisema Rais Kikwete angeunda tume hiyo na Waziri Nchimbi na IGP Said Mwema wanatakiwa kujiuzulu ili kupisha uchunguzi akidai kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba walitoa amri ya mauaji hayo.
“Dk Nchimbi anatakiwa kumuiga Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi ambaye alijiuzulu akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani baada ya kutokea mauaji, akijiuzulu atajijengea heshima tofauti na sasa kwani wananchi wamesikitishwa na mauaji hayo,” alisema Lissu.


Mwanasheria wa Chadema, Mabere Marando alidai kwamba kuna mkakati uliowekwa na Serikali wa kukidhoofisha Chadema baada ya kuonekana kwamba ni tishio kwa CCM.

Mbali na Chadema, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), pia limesema halina imani na kamati hiyo likisema imekuwa kawaida kwa Serikali kuunda tume ambazo hazileti ripoti kwa wananchi.
“Tume zimekuwa zikiundwa bila faida yoyote, huku zikipewa muda kuchunguza yaliyotokea lakini matokeo yake huwa hakuna ripoti wanayorudisha,” alisema Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta, Hezron Kaaya.


Kaaya alisema tume zimekuwa zikiundwa na kuigharimu Serikali fedha nyingi za walipa kodi, lakini ripoti zake zinaendelea kuwa siri.

Imeandikwa na Habiel Chidawali, Dodoma, Hamida Sharrif Morogoro, na Tumaini Msowoya, Iringa na Lasteck Alfred na Juliana Malondo.

Chanzo -
http://www.mwananchi.co.tz
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MANUMBA ASUSIWA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI IRINGA

Wanahabari wa Iringa Wakitoka nje ya ofisi

Wanahabari wa Iringa mchana wa leo wamegoma kupokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa kifo cha Mwandishi Daudi Mwangosi, aliyeuawa juzi jumapili katika mkutano wa ndani wa Chadema uliokuwa ufanyike katika kijiji cha Nyololo Iringa. Mkuu huyo alikataa shariti la wandishi la kumtaka atoe taarifa hiyo bila kuwepo kwa polisi yeyote katika mkutano huo. Kitendo hicho cha mkuu huyo kukataa shariti  la wanahabari kikapelekea waandishi kutoka nje ya ukumbi huo.Hivyo zoezi hilo kushindikana.

Picha na habari , Said Ng'amilo. Mjengwablog


[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

CCM yapumulia mashine




•  AJALI YA MV SKAGIT, URAIS 2015

VYAITESA

na Mwandishi wetu

UPEPO wa mabadiliko ya kisiasa

uliozikumba nchi nyingi duniani,

unaelekea kukiathiri Chama Cha

Mapinduzi (CCM) ambacho sasa

kinahaha kujinusuru kung’oka

madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa

mwaka 2015.

Chama tawala hivi sasa kina

msuguano mkubwa wa kiuongozi

ambapo baadhi ya viongozi wake

wamekuwa wakimshutumu Katibu

Mkuu, Willison Mukama, kwa

kukwamisha mikakati ya kujiimarisha

na kurejesha matumiani yaliyofifia

miongoni mwa wanachama wake.

Licha ya Katibu wa Itikadi na Uenezi,

Nape Nnauye, wiki hii kukanusha

kutokuwa na msuguano na Mukama,

makada wa chama hicho

wamelidokeza Tanzania Daima

Jumapili, kuwa vita ya makundi ya

kuwania uongozi na ile ya ufisadi

inakitesa chama hicho.

Mnyukano wa kisiasa unaonekana

wazi hivi sasa ni baina ya Waziri wa

Mambo ya Nje na Ushirikiano wa

Kimataifa, Bernard Membe, dhidi ya

kundi linalomuunga mkono aliyekuwa

Waziri Mkuu, Edward Lowassa,

anayetajwa kutaka kuwania urais

katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka

2015.

Wakati hali ya mambo ikionekana

kutokuwa nzuri ndani ya chama hicho,

nguvu kubwa sasa imehamishiwa

kwenye Bunge kwa lengo la

kuwadhibiti wabunge wa CHADEMA

ambao wanaelezwa kutishia uhai wa

chama hicho.

Makada wa CCM wamedokeza kuwa

wamebaini wabunge wa CHADEMA

mwaka 2005-2010 walilitumia vizuri

Bunge kujenga hoja za msingi ambazo

ziliwasaidia kujijenga na hatimaye

kupata wabunge 22 wa majimbo

kutoka watano.

Waliongeza kuwa kutokana na kubaini

jambo hilo, chama hicho kimeamuap

‘kuzishughulikia’ hoja zinazotolewa na

CHADEMA bila kujali kama zina

masilahi kwa taifa au la.

Inadaiwa kuwa viongozi wa Bunge

nao wamepewa maelekezo ya

kukisaidia chama chao hasa

wanapoona kuna hoja zinazoelekea

kuwapatia umaarufu wabunge wa

CHADEMA.

Tanzania Daima Jumapili,

limedokezwa kuwa pamoja na

maelekezo hayo baadhi ya viongozi

wa Bunge wameonekana kushindwa

kukisaidia chama tawala kwa sababu

ya kutozijua ipasavyo kanuni, hivyo

kutumia ubavu kukataa jambo

linalotolewa na wapinzani, hivyo

kuwaongezea umaarufu.

Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai,

anatuhumiwa kutoa fursa zaidi kwa

wabunge wa CCM kurudia maneno ya

dharau na lugha ya kuudhi dhidi ya

wapinzani.

Kiongozi huyo pia juzi alionesha

‘ukada’ wake pale alipojifanya kukosea

jina la Mbunge wa Viti Maalumu, Rose

Kamili, kwa kumuita Rose Kamili Slaa,

ilhali akijua mbunge huyo

alishatarikiana na Dk. Slaa.

Hata hivyo CCM hivi sasa pia

kinakabiliana na wakati mgumu wa

kushutumiwa kushindwa

kuwachukulia hatua watendaji wake

wanaobainika kufanya uzembe katika

shughuli zao za kila siku.

Ajali ya mv Spice Islanders iliyotokea

mwaka jana na mv Skagit iliyotokea

wiki iliyopita inadaiwa ilichangiwa na

uzembe wa wataalamu kwa

kushindwa kukagua ubora wake.

Serikali ya CCM pia inalaumiwa kwa

kushindwa kuwa na vifaa vya kisasa

vya uokoaji licha ya kila mara

kukumbwa na matukio ya ajali za

baharini na ziwani.

Katika ajali hizo mbili za majini

zilizopoteza maisha ya Watanzania

zaidi ya 400, serikali ya CCM

inalaumiwa kwa kushindwa

kusimamia sheria za usafiri wa majini

na kuficha taarifa ya uchunguzi wa

ajali ya awali.

Mmoja wa wabunge wa CCM ambaye

jina lake limehifadhiwa, aliilaumu

serikali kwa kuunda tume kuchunguza

ajali ya mv Bukoba na Spice Islanders,

lakini haikutoa matokeo ya uchunguzi

huo.

“Serikali iliunda tume kuchunguza ajali

ya awali ya mv Spice Islanders na mv

Bukoba lakini ikaficha matokeo ya

uchunguzi wake. Leo imetokea ajali

nyingine na binafsi naamini kama

matokeo ya uchunguzi wa awali

yangetolewa, bila shaka ajali ya juzi

ingeepukika,” alisema kada huyo.

Kufichwa kwa matokeo ya uchunguzi

wa ajali za awali za majini,

kumeelezwa kuwa ndiyo sababu ya

Spika wa Bunge, Anne Makinda,

kuzima hoja za wabunge wa kambi ya

upinzani walioungana na wabunge

wote wa Zanzibar kutaka kujadili ajali

ya mv Skagit iliyosababisha vifo vya

zaidi ya watu 150.

Chanzo: FreeMedia
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

UTORO WA WABUNGE WAKWAMISHA BAJETI




•  WAPINZANI WANG’ANG’ANIA

ISIPITISHWE

na Salehe Mohamed, Dodoma

UTORO wa wabunge uliokemewa na

Spika wa Bunge, Anne Makinda, wiki

iliyopita jana ulikwamisha kupitishwa

kwa bajeti ya Wizara ya Kilimo,

Chakula na Ushirika.

Wiki iliyopita Makinda alisema utoro

kwa wabunge hivi sasa umekithiri na

akaonya kuwa kama wataendelea na

tabia hiyo ipo siku watakwamisha

upitishaji wa bajeti ya wizara husika.

Utabiri huo wa Spika Makinda, jana

ulitimia baada ya wabunge hasa wa

kambi ya upinzani kuibua hoja ya

kukwamisha upitishwaji wa bajeti ya

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika

kwa mwaka 2012/2013 kutokana na

uchache wa wabunge.

Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia

(NCCR-Mageuzi), ndiye aliyekuwa wa

kwanza kutoa hoja kwa kutumia

kanuni ya 112 ambapo alitaka bajeti

hiyo isipitishwe kwa kuwa wabunge

waliopo hawajafikia nusu ya wabunge

wote.

“Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni

inataka Bajeti ipitishwe ikiwa idadi ya

wabunge waliohudhuria itafikia nusu

ya wabunge wote.

“Hapa tulipo mimi nimeshahesabu

mara mbili wabunge wote hatuzidi

110, na tunajua idadi ya wabunge

wote ni 352 na nusu yake ni wabunge

175, ili tutende haki nakuomba

uhesabu idadi ya wabunge waliopo

kabla ya kupitisha bajeti hii ili

tuwatendee haki Watanzania,”

alisema.

Baada ya hapo alisimama Mbunge wa

Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-

Mageuzi) akitumia kanuni ya 77 (1) na

(2) kuwa wabunge waliopo hawafikii

nusu ya wabunge wote.

“Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni ya

77 (1). Akidi kwa kila kikao cha Bunge

wakati wa kufanya maamuzi itakuwa ni

nusu ya wabunge wote, kama

ilivyofafanuliwa katika ibara ya 94 ya

Katiba, isipokuwa kwamba idadi hiyo

haitahusu hoja kuhusu uamuzi wa

kubadilisha masharti yoyote ya Katiba

kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba.

“Mbunge yeyote aliyehudhuria

anaweza kumjulisha Spika kwamba,

wabunge waliopo ni pungufu ya akidi

inayohitajika kwa ajili ya shughuli

inayoendelea.

“Kwa maana hiyo, Mheshimiwa Naibu

Spika, nasisitiza kuwa hatufiki nusu

humu ndani,” alisema.

Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses

Machali (NCCR-Mageuzi) naye

alisisitiza kanuni hiyo hiyo kipengele

cha tatu. “Endapo Spika ataridhika

kwamba kweli idadi ya wabunge walio

ndani ya Ukumbi wa Bunge ni

pungufu ya akidi inayohitajika basi

atasimamisha shughuli za Bunge kwa

muda atakaoutaja na atamwagiza

katibu kupiga kengele.”

Naibu Spika Job Ndugai, alisema idadi

hiyo inatakiwa wakati wa kupiga kura

ya mwisho ya kuipitisha bajeti hiyo si

wakati wa hatua za awali za kamati ya

matumizi.

Kauli hiyo ilimfanya Mnadhimu wa

Kambi Rasmi ya Upinzani, Tundu

Lissu, asimame na kutaka kiti cha

Spika kisiliburuze Bunge kwa kukiuka

kanuni na kuliomba Bunge liahirishe

shughuli hiyo.

Hata hivyo Ndugai hakukubaliana na

kauli ya Lissu. Ndugai huku akisema

kuahirisha shughuli za Bunge ni

gharama kubwa, alichukua muda

kuamua jambo hilo.

Ndugai aliamuru Kamati ya matumizi

iendelee huku Waziri wa Nchi Ofisi ya

Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge),

William Lukuvi, alitoka nje

kuwahamasisha wabunge warejee

ukumbini. Mbali na juhudi za Waziri

Lukuvi pia kengele ilikuwa ikipigwa nje

ya ukumbi wa Bunge kuwahamasisha

warejee ukumbini.

Juhudi zakwama

Pamoja na jitihada za viongozi

mbalimbali wa serikali na Bunge

kuhakikisha idadi ya wabunge inafika

nusu, jambo hilo lilishindikana na

ndipo Ndugai alipoamua kuahirisha

shughuli za Bunge.

“Ni Vizuri wananchi waelewe kuwa

tuna huu msiba wa kitaifa

unaoendelea Zanzibar kuna wabunge

wenzetu wako kule Zanzibar hasa

kutoka Zanzibar kwa ruhusa ya

Spika…, kuna mawaziri na manaibu

wapo kule na wengine wako kule kwa

shughuli maalumu.

“Kuna wabunge kadhaa ambao mimi

mwenyewe nimewaruhusu wapo

kwenye msiba wa mazishi ya mama

wa mbunge mwenzetu, Mike Lekule

Laizer (CCM).”

Wakati Ndugai akiendelea kutoa

ufafanuzi huo, wabunge wa upinzani

walikuwa wakitoa kauli na kugonga

meza kuonesha kupinga utetezi huo.

Vitendo hivyo vilimfanya Ndugai

kuwataka wamsikilize badala ya kupiga

kelele ambazo haziwasaidii, kwakuwa

kiti cha Spika hakiwezi kumkandamiza

mtu.

“Nawaombeni ndugu zangu

tunaposikilizana kama watu wazima…

tupeane nafasi, mnalolitaka litakuwa

…..mkisema nyinyi nawapa

nafasi….mimi nikisema mnaanza

kupiga kelele.

“Inanisikitisha sana tunapovunjiana

heshima, tunakuwa kama watoto

wadogo, mimi sidhani kama

inatujengea heshima mahali popote

katika nchi yetu, tunafanya jambo la

msingi la taifa,” alisema.

Alisema kwa busara alizonazo

ameamua kuahirisha kikao hicho,

hatua ya kamati ya Bunge zima hadi

Jumatatu (kesho).

Baada ya kauli hiyo wabunge wengi

hasa wa upinzani walikuwa wakipiga

meza kwa kushangilia ‘ushindi’

walioupata.

NCCR-Mageuzi wakomalia

Mara baada ya Bunge kumalizika

wabunge wa NCCR-Mageuzi

walikutana na waandishi wa habari na

kuweka bayana kuwa hivi sasa

wanafanya uchunguzi kujua ni vikao

gani vilifanyika bila idadi ya wabunge

kutimia, baada ya hapo wapeleke hoja

kutaka maamuzi yaliyofikiwa

yatenguliwe.

Mbunge wa Kasulu Kusini, David

Kafulila, alisema maamuzi mengi

yamekuwa yakifanywa bila akidi

kutimia, jambo ambalo ni hatari kwa

maendeleo ya taifa.

“Tutaomba Spika atupe orodha ya

wabunge waliohudhuria katika kikao

hiki cha Bajeti na tukibaini tutaomba

maamuzi yaliyoafikiwa yatenguliwe,”

alisema.

Chanzo FreeMedia
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Rais Kikwete Akutana na Kufanya Mazungumzo na Profesa Ntumra Luaba Alphonce, Katibu Mtendaji wa Umoja wa Nchi za Maziwa Makuu wa (International Conference on Great Lakes Region ICGLR) mjini Bujumbura, Burundi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete amesema kuwa
hali ya mashariki mwa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo (DRC)
inatia wasiwasi na hivyo Tanzania
inafuatilia kwa makini hali
inavyoendelea katika eneo hilo la
nchi hiyo jirani.

Aidha, Rais Kikwete amesema
kuwa Tanzania ingependa kuona
hali ya amani inarejea katika DRC
kwa sababu nchi hiyo inahitaji
kupata muda wa amani ili
waelekeze nguvu zake kwenye
maendeleo badala ya kupigana.
Rais Kikwete amesema hayo jana,
Jumanne, Juni 3, 2012, wakati
alipokutana na kufanya
mazungumzo na Profesa Ntumra
Luaba Alphonce, Katibu Mtendaji
wa Umoja wa Nchi za Maziwa
Makuu wa International
Conference on Great Lakes Region
(ICGLR) kwenye Hoteli ya Roca
Golf mjini Bujumbura, Burundi.
Rais Kikwete akifuatana na Mama
Salma Kikwete alikuwa mjini
Bujumbura kushiriki katika
Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa
Burundi na kurejea nyumbani jana,
3 Juni, 2012. Kabla ya kuja hapa,
Rais Kikwete alikuwa mjini Kigali,
Rwanda, kushiriki katika sherehe
za namna hiyo zilizofanyika Julai
Mosi, mwaka huu. Rwanda na
Burundi zilipata uhuru kutoka kwa
Wabelgiji Julai Mosi na Julai 2,
mwaka 1962.

Rais Kikwete amemwambia Katibu
Mtendaji huyo: “ Kwa hakika hali
mashariki mwa Congo inatutia
wasiwasi mkubwa na Tanzania
inafuatilia kwa makini hali hiyo.
Congo imekuwa katika vita muda
mrefu kupita kiasi kwa sababu
tokea mwaka 1997 imekuwa katika
vita mfululizo.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Wakati
umefika kwa Congo kutulia ili
nguvu inayoingia katika
mapambano na vita ielekezwe
katika maendeleo ya wananchi wa
nchi hiyo.”

Rais Kikwete pia ameunga mkono
wazo la kuitishwa kwa mkutano
wa mawaziri wa nchi wanachama
wa ICGLR ili kujadili hali ilivyo
katika mashariki mwa Congo
kufuatia ombi la DRC kutaka
kuitishwa kwa mkutano huo.
Hali katika mashariki mwa Congo
imeanza kutia wasiwasi baada ya
kikundi cha waasi wa Serikali ya
nchi hiyo wakiongozwa na jambazi
la kivita John Bosco Ntaganda
kuanza tena harakati zake za
kivita dhidi ya Serikali ya Rais
Joseph Kabila.

Usiku wa jana, Jumanne, Julai 3,
2012, alikutana na kufanya
mazungumzo na Rais wa
DRC,Mheshimiwa Kabila kuhusu
hali ilivyo mashariki mwa DRC.
Wakati akiwa Kigali,
Rwanda,mwishoni mwa wiki, Rais
Kikwete pia alikutana na kufanya
mazungumzo na Rais Paul Kagame
kuhusu hali ilivyo mashariki mwa
DRC.

Aidha, usiku huo huo wa kuamkia
jana, Rais Kikwete alikutana na
kufanya mazungumzo na Naibu
Waziri Mkuu wa Ubelgiji,
Mheshimiwa Didier Reynders
ambaye pia anahusika na masuala
ya nchi za nje, biashara ya nje na
masuala ya Umoja wa Ulaya (EU).
Katika mazungumzo Rais Kikwete
na Mheshimiwa Reynders
walizungumzia hali ya mashariki
mwa Congo pamoja na mchakato
wa ushirikiano ndani ya Jumuia ya
Afrika Mashariki (EAC).

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya
Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
4 Julai, 2012


[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

WAZIRI WA USALAMA NA ULINIZI KENYA PROF. GEORGE SAITOTI AFARIKI KWA AJALI YA HELIKOPTER


Waziri wa Usalama wa ndani Profesa George Saitoti na Naibu wake Orwa Ojode wamefariki dunia katika ajali ya helikopta ya polisi iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Kibiku, karibu na mji wa Ngong takriban kilometa ishirini kutoka mji mkuu wa Nairobi.

Abiria wote sita, wakiwemo marubani wawili na walinzi wa mawaziri hao waliokuwa kwenye helikopta hiyo wamefariki dunia na miili yao kuteketezwa kwa kiasi cha kutoweza kutambulika.


Kilichosababisha ajali hiyo bado hakijabainika. Bwana Saitoti na maafisa wengine wa juu katika wizara ya usalama wa ndani walikuwa wakielekea katika eneo la Sotik kwa mkutano wa usalama. Saitoti alikuwa miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Kenya waliokuwa wakipania kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.


Walioshuhudia ajali hiyo wamesema waliona helikota hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika msitu wa Ngong.
Polisi wamezingira eneo la ajali hiyo na kamishna wa polisi Mathew Iteere aliyepo katika eneo la ajali anatarajiwa kutoa taarifa kamili kuhusiana na ajali hiyo.
Ajali hiyo ya helikopta imetokea katika siku ambapo Kenya inaadhimisha miaka minne tangu kutokea ajali ya ndege iliyowauwa mawaziri wengine wa serikali, Kipkalya Kones na Lorna Laboso.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AFUNGUA KIWANDA CHA NYUKI KIBAHA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua mitambo baada ya kufunguza kiwanda cha kusindika asali cha  Organic Honey katika kijiji cha Visiga  mkoani Pwani  kinachomilikiwa na Kampuni ya  Boleyn  International, Juni 9, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

RAIS KIKWETE AZUIWA KUSOMA RIPOTI



NI YA KUJITATHIMINI KATIKA MKUTANO WA AU,KISA MADENI

Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete amezuiwa kuwasilisha taarifa ya Tanzania kuhusu utekelezaji wa mpango wa Mpango wa kujitathmini wa Umoja wa Afrika (APRM), kwa sababu ya madeni makubwa yanayotokana na kutowasilishwa kwa michango kwa ajili ya uendeshaji wa sekretarieti ya mpango huo.
Tanzania inadaiwa kiasi cha Dola za Marekani 800,000 sawa na Sh1.258 bilioni kwa kuzingatia viwango vya kubadilisha fedha (exchange rate) vya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambavyo ni wastani wa Sh1, 572.87 dhidi ya Dola ya Marekani.
Deni hilo ambalo ni malimbikizo ya ada ya Dola 100,000 kila mwaka kwa miaka minane mfululilizo tangu mwaka 2005 ni kashfa kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inayoongozwa na Waziri Benard Membe, ambayo mpango wa APRM unatekelezwa chini yake.
Julai 22 mwaka jana, wakati akiwasilisha makadirio ya wizara yake, Membe alisema taarifa kamili ya mchakato huo hapa nchini ilitarajiwa kuwa imekamilika na kuwasilishwa katika Mkutano Mkuu wa nchi wanachama wa APRM Julai, 2012.
Ni kwa mantiki hiyo, Rais Kikwete alitarajiwa kuwasilisha ripoti ya Tanzania kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika (AU) utakaofanyika Lilongwe, Malawi Julai 10 mwaka huu, lakini habari zinasema deni hilo limekwaza mpango huo.
Katibu Mtendaji wa APRM Tanzania, Rehema Twalib alisema jana: “Ni kweli kwamba tunadaiwa Dola 800,000 ambazo ni kama Sh1.2 bilioni na kidogo hivi na hizo ni malimbikizo ya mwaka huu wa 2012 na miaka mingine ya nyuma kwa sababu kila mwaka tunatakiwa kulipa Dola 100,000.”
Habari zilizopatikana baadaye na kuthibitishwa na Twalib zinasema tayari APRM Tanzania imepokea waraka kutoka Sekretarieti ya APRM na AU makao makuu kwamba ripoti ya Tanzania haitaweza kuwasilishwa katika mkutano huo wa Lilongwe.
“APRM nadhani wamepokea barua kutoka makao makuu kwamba Rais wetu hataweza kuwasilisha ripoti ya Tanzania, lakini hawa jamaa ni wajanja sana hawakueleza sababu ila wameambatanisha na orodha ya madeni tunayodaiwa kama nchi,”alisema mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na kuongeza:
“Hii ni aibu kwa Tanzania, wenzetu wanatushangaa kwamba sisi tumekuwa nyuma katika mambo haya yanayohusu Utawala Bora wakati sisi ndiyo tulitarajiwa kuwa msitari wa mbele kuliko wengine.”
Twalib katika maelezo yake alikiri kwamba Rais Kikwete hatawasilisha ripoti ya Tanzania kwenye mkutano huo wa Lilongwe lakini akasema hilo halihusiani moja kwa moja na deni nchi inalodaiwa.
“Kweli walileta taarifa hiyo kwamba taarifa yetu haitawasilishwa kwenye mkutano ujao, lakini ni kwa sababu ya mchakato wenyewe kuwa mrefu, lazima ipitie kwenye ngazi mbalimbali na kwa kungalia muda uliobaki pengine waliona kuwa hautatosha kukamilisha hatua zote,” alisema Katibu Mtendaji huyo.
Sehemu ya taarifa ya APRM Tanzania iliyowasilishwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (NEC- CCM), Mei 15 mwaka huu, mjini Dodoma inaeleza kuwapo kwa kusudio miongoni mwa nchi zinazoshiriki mchakato wa APRM kuziengua zile zisizolipa madeni yake.
“Tanzania imeshindwa kulipa ada zake za kila mwaka kwa Sekretarieti ya AU/APRM kwa miaka saba iliyopita. Baadhi ya nchi zimeanza wanachama wa mchakato huu zimeanza kujenga hoja kwamba nchi kama Tanzania ziondolewe kwenye mchakato huu,”inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Hata hivyo, Twalib alisema licha ya kwamba Tanzania inapaswa kulipa madeni yake, lakini hakuna kipengele chochote kinachoipa Sekretarieti ya APRM mamlaka ya kuizuia nchi kutathminiwa katika mkutano wa wakuu wa nchi.
Alikiri kuwa deni hilo linachafua taswira ya Tanzania mbele ya nchi nyingine na kwamba lazima yalipwe kwani ilijiunga kwa hiari na kusaini makubaliano ya kutoa michango husika.

Deni la Tanzania
Rais Kikwete alipata taarifa za Tanzania kudaiwa na APRM katika kikao cha (NEC- CCM) Mei 15, mwaka huu mjini Dodoma na inaelezwa kwamba zilimsutua.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema kuwa Rais alishangazwa na taarifa hizo hivyo kuagiza mchakato wa malipo ya deni hilo uanze mara moja: “Kweli Rais alionyesha kushangazwa na deni hilo na aliagiza kwamba fedha hizo zilipwe kesho yake,” alisema mmoja wa wajumbe wa NEC.
Hata hivyo, haifahamiki iwapo agizo hilo la Rais lilitekelezwa au la kwani wiki mbili tangu atoe maelekezo hayo ndipo APRM Tanzania walipopata taarifa kutoka AU kwamba ripoti ya Tanzania haitaweza kuwasilishwa.

Taarifa iliyowasilishwa NEC ambayo Mwananchi limeiona, inaonyesha kuwa katika mwaka wa fedha wa 2012/13 APRM Tanzania wameomba kuidhinishiwa kiasi cha Sh5.194 bilioni kwa ajili ya kugharamia kazi zake lakini maombi yaliyowasilishwa Hazina na wizara kwa ajili ya mango huo ni Sh1.149 bilioni tu.
“Kwa upande mwingine kama fedha tulizoomba Sh5,194, 204,304 zingeidhinishwa, tungeweza kutekeleza majukumu yetu kama yalivyopangwa kwa kuzingatia mahitaji ya kitaifa ikiwa ni pamoja na kulipa limbikizo la deni la Sh1.280 bilioni ambalo halijalipwa kwa miaka saba,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo inaonyesha kwamba kiwango kinachopendekezwa kuidhinishwa na Bunge kinaweza kutosheleza kugharamia kazi za mchakato wa APRM nchini kwa miezi mitatu na kidogo ikilinganishwa na kile kilichoidhinishwa katika mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, mwaka huu ambacho ni Sh 2.04 bilioni.
Tanzania pia inatajwa kwenye taarifa ya Sekretarieti ya APRM ya mwaka 2010 kwamba ni miongoni mwa nchi ambazo zimewahi kuwasilisha michango yake mara moja tu tangu iliposaini na kuridhia kushiriki kwenye mchakato wa kutathminiwa utendaji wake.

Nchi nyingine ambayo imewahi kulipa michango yake mara moja ni Sierra Leone wakati Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Djibouti, Sudani na visiwa vya Sao Tome na Principe hazijawahi kutoa mchango wowote.

Tanzania ni nchi pekee katika kanda ya Afrika Mashariki na Kati inayodaiwa fedha nyingi ililinganishwa na majirani zake ambazo zinadaiwa kiasi cha fedha kwa Dola za Marekani kwenye mabano, Rwanda (300,000), Zambia (200,000), Kenya (100,000) na Uganda (400,000).
Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ezekia Wenje katika maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni, Julai 22 mwaka jana alihoji sababu za Serikali kushindwa kulipa deni hilo ambalo alisema linalitia aibu taifa.

“Deni la nchi yetu katika Sekretarieti ya APRM ngazi ya Bara la Afrika na malimbikizo yanafikia Sh 1.07 bilioni. Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuthibitisha taarifa hizi na kujieleza ni kwa nini kwa kipindi chote hicho haikulipa ada ya uanachama APRM na lini italipa fedha hizo, kwani hii ni aibu kubwa kwa Taifa,” alisema Wenje.

APRM Tanzania
Mchakato wa kujitathini wa nchi za Afrika ulibuniwa na viongozi wa Afrika mwaka 2002, taasisi hiyo ilianza rasmi mwaka 2003 baada ya idadi ya wanachama iliyotakiwa kusaini mkataba huo kutimia.
Kwa upande wa Tanzania, Kamati ilibaini Taarifa Rasmi za Bunge (Hansard) zinaonyesha kuwa mpango huo uliridhiwa na Bunge la Nane, Februari 1, 2005, katika kikao cha Kumi cha Mkutano wake wa 14 na kupitisha Azimio la kuridhia Mkataba wa Tanzania kujiunga na Utaratibu wa African Peer Review Mechanism.

Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama katika taarifa yake mwaka jana ilisema: “Kuna umuhimu mkubwa kwa Serikali kutenga fedha kwa ajili ya mchakato huo sanjari na kulipia michango na ada ya uanachama kwa wakati.”

Hivyo hatua ya Tanzania kuzuiwa kuwasilisha taarifa yake kunaifanya iendelee kuchelewa zaidi kwani tayari muda uliotarajiwa kukamilisha mchakato huo ulikwishapita.

Wenje katika hotuba ya upinzani alibainisha kwamba: “Ni dhahiri kuwa nchi yetu imechelewa sana. Ni dhahiri kuwa Serikali haikutimiza wajibu wake kuhakikisha mchakato huu wa kujitathmini unatekelezwa kwa wakati kwani takriban miaka sita imepita tangu Bunge hili lipitishe uamuzi wa kuingia kwenye mchakato wa APRM, lakini hadi leo hatujaweza kupata ripoti ya mwisho ya APRM kuhusu nchi yetu.”

“Kwa kawaida kazi ya kujitathmini inapaswa kufanyika mara moja ndani ya kila miaka mitano, lakini kwa Tanzania huu ni mwaka wa saba bila kupatikana kwa ripoti ya mwisho. Nchi nyingine kama Ghana,Uganda na Rwanda tayari zimejitathimini na kupata ripoti zao za mwisho.”



CHANZO: MWANANCHI
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

BAJETI YA SERIKALI 2012/2013 YAKADIRIW KUWA SHILINGI TRILIONI 15


BAJETI ya Serikali ya mwaka 2012/2013 inatarajiwa kutumia Sh15 trilioni katika vipaumbele saba ikilinganishwa na Sh13.5 trilioni zilizotengwa mwaka 2011/12.Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa aliileza Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi kuwa matumizi ya kawaida ya Serikali yanatarajiwa kuwa Sh10 trilioni na fedha za maendeleo ni Sh5 trilioni.


Dk Mgimwa alieleza  kuwa kipaumbele cha kwanza katika Bajeti yake ya kwanza tangu kuteuliwa hiyo ni miundombinu. Kwa mujibu wa waziri huyo, miundombinu imegawanyika katika makundi manne ya reli, umeme, maji salama, usafirishaji na uchukuzi ambavyo vimetengewa jumla ya Sh4.5 trilioni. Vipaumbele vingine vya Serikali ni kilimo, viwanda, rasilimali watu, huduma za jamii, utalii, biashara ya ndani na nje na huduma za fedha.


Habari kutoka ndani ya kikao hicho zilisema kuwa katika bajeti hiyo, fedha zilizopelekwa Wizara ya Uchukuzi kwa ajili miradi ya maendeleo ni Sh252 bilioni huku sekta ya usafiri wa reli ikitarajiwa kutumia Sh130 bilioni. Katika Bajeti hiyo ya maendeleo, Wizara ya Ujenzi imetengewa Sh693 bilioni, wakati sekta ya nishati ikiwa nayo imepewa umuhimu na mradi wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka mikoa ya kusini umetengewa Sh325 bilioni. Mwelekeo huo wa bajeti unaonyesha pia kwamba, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imetengewa jumla ya Sh364 bilioni.


Serikali Kuuza mashangingi 
Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho, zilisema katika mkakati wa kubana matumizi, Serikali itapunguza matumizi ya magari ya kifahari kwa kiwango kikubwa.  Katika hatua hiyo, inatarajiwa pia kupiga mnada baadhi ya magari hayo yanayotumiwa na mawaziri, manaibu waziri, makatibu wakuu na wakurugenzi na kununua magari madogo yenye gharama nafuu.  Hata hivyo, chanzo chetu kilisema waziri huyo hakufafanua suala hilo akisema atalizungumza zaidi wakati wa kuwasilisha Bajeti hiyo Mjini Dodoma.


Takwimu za Serikali za mwaka juzi, zilionyesha kuwa Serikali Kuu hadi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) ilikuwa ikimiliki magari 40,000, kati yake 11,000 yakiwa ya kifahari.Tayari Wizara ya Ujenzi kupitia timu ya wataalamu mwaka Aprili, 2007 ilitoa ripoti ya namna bora ya kupanga matumizi ya magari ya Serikali kwa kuangalia kila daraja la kiongozi, lakini ripoti hiyo iliishia mezani kwa aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo.


Baadhi ya wabunge wa CCM wanatarajia kuibana Serikali katika Bunge lijalo wakidai kuwa imeshindwa kutekeleza kwa ukamilifu Bajeti ya mwaka jana pamoja na kuwawajibisha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi.
Katika mkutano uliopita, wabunge waliibana Serikali wakitaka mawaziri wanane, manaibu waziri wawili na watumishi wengine wa umma waliotajwa katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), wawajibishwe. Lakini wabunge hao wamesema Rais Jakaya Kikwete aliwafuta kazi mawaziri sita na kuwahamisha wizara wawili na kuwang’oa manaibu waziri wawili miongoni mwa waliotajwa na hawajaona juhudi za kuwawajibisha watuhumiwa wengine.


Mawaziri waliofutwa kazi ni William Ngeleja (Nishati na Madini), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), Omari Nundu (Uchukuzi), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara) na Mustafa Mkulo (Fedha). Waliohamishwa wizara ni Profesa Jumanne Maghembe (Kilimo) kwenda Maji na George Mkuchika (Tamisemi) kwenda Ofisi ya Rais, Utawala Bora. Manaibu Waziri waliotemwa ni Dk Lucy Nkya (Afya na Ustawi wa Jamii) na Athumani Mfutakamba (Miundombinu).
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

JK ASALIMIANA NA BECKHAM AIRPORT HEATHROW


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakisalimiana na mchezaji soka nyota wa Uingereza anayechezea Los angeles Galaxy ya Marekani,   David Beckham,  walipokutana uwanja wa ndege wa Heathrow jijini London Jumatano, muda mfupi kabla ya Rais Kikwete na Mama Salma kuelekea Washington DC kuhudhuria mkutano wa G8 kwa mwaliko wa Rais Barak Obama wa Marekani. Bekham ameonesha nia ya kutembelea Tanzania kama mtalii siku za karibuni na Rais Kikwete amemkaribisha kwa mikono miwili, akimhakikishia kwamba licha ya kuwa na mashabiki wengi ambao watafurahi kumuona pia atafurahia vivutio kibao vya kitalii. 
Picha na Amos Msanjila

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»