Showing posts with label Mama salma. Show all posts
Showing posts with label Mama salma. Show all posts

MWENYEKITI WA WAMA MAMA SALMA KIKWETE AKUTANA NA UJUMBE WA G E CORPORATE KUTOKA MAREKANI


 Picha ya pamoja baada ya Mwenyekiti  wa Taasisi ya WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete kumaliza mazungumzo na ujumbe kutoka Marekani  pamoja na ungozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii
 Mama Salma Kikwete akiongea na wageni baada ya kumaliza mazungumzo.
 Katibu wa Taasisi ya WAMA Daudi Nasibu (kulia) akiagana na  Mjumbe kutoka Marekani wa Taasisi ya E G Health (kushoto) Reza Bundy baada ya kumaliza mazumgumzo na Mwenyekiti  wa Taasisi ya WAMA Mama Salma Kikwete, (pichani hayupo) Mazungumzo hayo pia yamewahusisha wataalamu kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Blandina Nyoni hayupo pichani.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya WAMA Zakhia Mehgji (kulia) akibadilishana mawazo katika ofisi za WAMA jijini Dar es Salaam na wajumbe  wa taasisi ya E G Health kutoka Marekani (kushoto)ni Director, Global Programs healthymogination Joneen Uzzeli na (aliesimama katikati) ni Co- Director of African First Ladies Fellowship Program  Cora Neumann, wakati ujumbe huo ulipokwenda kumtembelea Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (hayupo pichani ) na kuzungumzia jinsi ya kusaidia kuwaletea vifaa tiba kwaajili ya kusaidia kupunza vifo ya wakinamama na watoto wachanga nchini . 
Katibu wa Taasisi ya WAMA Daudi Nasibu (aliesimama) akitoa taarifa kwa wageni  pamoja na uongozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii katika Ofisi za WAMA walipokutana na Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mama Salma Kikwete kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu kusaidia kuleta vifaa tiba kwaajili ya jitihada  za kupunguza vifo vya wakinamama na watoto wachanga nchini, Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MAMA SALMA KIKWETE ASHIRIKI KUAGA MWILI WA MAREHEMU MAMA HAN BING JIJINI DAR LEO


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA , akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Mama Han Bing mke wa Mwenyekiti wa jumuiya ya wafanya biashara wa kichina nchini Tanzania aliefariki siku kadhaa zilizopita jijini Dar es Salaam kwa kuuwawa na majambazi wasiojulikana.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete,akiwa na viongozi mbali mbali kwenye ibada ya kumuombea Marehemu
Picha ya Marehemu Mama Han Bing mke wa Mwenyekiti wa jumuiya ya wafanya biashara wa kichina nchini Tanzania
Kamanda wa kanda maaluum ya kipolisi ya Dar es Salaam,Suleiman Kova akiwapa pole wana jumuiya ya wachina waishio Tanzania jijini Dar es salaam wakati walipokwenda kuaga mwili wa Mama Han Bing alieuwawa na majambazi.
Wanajumuiya ya Kichina waishio nchini Tanzania wakiwa kwenye misa ya kumuombea Marehemu Mama Han Bing mke wa Mwenyekiti wa jumuiya ya wafanya biashara wa kichina nchini Tanzania
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpa pole Mume wa Marehemu,Bw. Bing ambaye alikuwa ni mwenye huzuni mkubwa sana wa kuondokewa na mke wake aliyeuwawa na Majambazi siku kadhaa zilizopita.
Mama Salma Kikwete akimfariji Mtoto wa Marehemu.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mh. Bernard Membe akitoa salamu za pole wa wafiwa na wanajumuiya ya kichina katika msiba huo.
Mume wa Marehemu (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na wanafamilia wengine kwenye misa ya kumuombea Marehemu.
Mmoja wa Kina Mama wa Kichina akilia kwa huzuni baada ya kuondokewa na ndugu yao.
Mmoja wa wanafamilia akimbembeleza mtoto wa Marehemu.
Picha na Mwanakombo Jumaa- Maelezo.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»