Showing posts with label mbunge. Show all posts
Showing posts with label mbunge. Show all posts

MBUNGE PETER MSIGWA ANUSURIKA KATIKA AJALI


Gari la mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa likiwa limeingia nyuma ya gari ambalo lilikuwa mbele yake kabla ya dereva wa gari hilo la mbele kuamua kurudi nyuma ghafla na kuligonga gari hilo la mbunge


Mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (chadema) leo amenusurika katika ajali ya gari baada ya gari lake kugongana na gari jingine ambalo lilikuwa mbele yake kabla ya wa dereva wa gari hilo ambalo lilikuwa likiingia barabara kuu kuamua kurudisha nyuma ghafla gari lake na kuligonga gari hilo na mbunge.

Tukio hilo limetokea leo majira ya mchana wakati mbunge Msigwa akitoka katika kuwatumikia wananchi wake wa jimbo hilo.

Hata hivyo katika ajali hiyo gari la mbunge Msigwa halikuharibika sana ukilinganisha na gari hilo lililo rudi nyuma na kumgonga.

HABARI NA PICHA KWA HISANI YA FRANCIS GODWIN BLOG
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MBUNGE WA JIMBO LA MBARALI MWALIMU KILUFI AACHIWA KWA DHAMANA NA MAHAKAMA YA HAKIMU MFAWIDHI WA WILAYA YA MBEYA. JANA


Mbunge wa jimbo la Mbarali(kushoto) Mwalimu Dickson Kilufi akisikiliza jambo kutoka kwa mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania daima, Bwana Gordon Kalulunga mara baada ya mbunge huyo kuachiwa kwa dhamana na mahakama ya Hakimu mfawidhi wa wilaya ya Mbeya ambapo alipandishwa kizimbani mwanzoni mwa wiki hili.


Mbunge wa jimbo la Mbarali Mwalimu Kilufi(katikati), akisalimiana na baadhi ya wananchi waliofika mahakamani kusikiliza kesi ya mbunge huyo, ambaye ameachiwa kwa dhamana na mahakama ya Hakimu mfawidhi wa wilaya ya Mbeya ambapo alipandishwa kizimbani mwanzoni mwa wiki hili.



Wananchi wakiwa nje ya mahakamani baada ya kumalizika kwa kesi ya Mbunge wa Jimbo la Mbarali Mwalimu Kilufi aliyeachiwa kwa dhamana na mahakama ya Hakimu mfawidhi wa wilaya ya Mbeya ambapo alipandishwa kizimbani mwanzoni mwa wiki hili.


Baadhi ya Wananchi wakitoka nje ya mahakamani baada ya kumalizika kwa kesi ya Mbunge wa Jimbo la Mbarali Mwalimu Kilufi aliyeachiwa kwa dhamana na mahakama ya Hakimu mfawidhi wa wilaya ya Mbeya ambapo alipandishwa kizimbani mwanzoni mwa wiki hili.


*****
Na mwandishi wetu
Mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya Modestus Kilufi mwenye umri wa miaka 51 kupitia tiketi ya CCM aliyepandishwa kizimbani mwanzoni mwa wiki hii katika Mahakama ya Hakimu mfawidhi wa wilaya ya Mbeya na kunyimwa dhamana amechiwa huru kwa dhamana.

Kilufi aliachiwa kwa dhamana jana asubuhi na mahakama hiyo na kuamuliwa kufika Mahakamani hapo Octoba 24 mwaka huu kuendelea kusikiliza shitaka linalomkabili la kutishia kuua.

Zaidi ya wananchi 25 walijitokeza kwa ajili ya kumdhamini Mbunge huyo lakini mahakama ilihitaji wadhamini wawili tu ambapo baada ya kuachiliwa huru, nje ya mahakama kulitawala shangwe huku wakili wake Simon Mwakolo akikataa kuzungumza na waandishi wa habari na kumkataza mteja wake kuzungumza lolote.

Baada ya hapo Mbunge huyo aliwaeleza wananchi hao na familia yake kuwa alikuwa ameitwa na uongozi wa CCM kauli iliyopingwa vibaya huku baadhi wakisikika kuwa walikuwa wapi kumsaidia tangu awali na walikuwa wanamwitia nini! Hali iliyoonesha kumkatisha tamaa na baadaye alipanda gari yake na kuondoka na kwenda ofisi za chama hicho.

Awali Mbunge huyo alifikishwa mahakanani kwa kosa la kumtishia kumzuru Jordan Masweve March 16 mwaka huu wilayani Mbarali.

Kosa hilo lilielezwa kuwa ni kinyume na kifungu cha sheria 189 cha mabadiliko ya sheria ya mwaka 2002 kifungu kidogo cha 2(a) sura ya 16 ambapo mshitakiwa alikana shitaka.

Kesi hiyo yenye namba CC/158/2011 baada ya mshitakiwa kukana shitaka linalomkabili, ndipo wakili wa Mbunge huyo Simon Mwakolo aliiomba mahakama hiyo dhamana kwa mteja wake lakini Mahakama ilikataa kasha akapelekwa rumande ya gereza la Ruanda ambako amekaa mahabusu kwa muda wa siku tatu.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MBUNGE WA JIMBO LA MBARALI KUFIKISHWA MAHAKAMANI JUMATATU.


Na mwandishi wetu
Mbunge wa Jimbo la Mbarali Mwalimu Dickson Kilufi atafikishwa mahakama ya mkoa wa Mbeya siku ya jumatatu tarehe Oktoaba 10, mwaka huu baada ya kudaiwa kutishia kuua kwa maneno Machi 15, mwaka huu katika Ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Mbarali.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amesema mbunge huyo amedhaminiwa baada ya kukamatwa juzi na kushikiliwa na Jeshi la polisi ambapo Mwanasheria wa serikali alikubali dhamana iliyotolewa jumamosi ya Oktoba 8, mwaka huu.

Mbunge Kilufi anadaiwa kumtishia kumuua Afisa mtendaji wa Kata ya Ruiwa Bwana Jordan Masweve mbele ya diwani wa kata hiyo Bwana Alex Mndamlage.

Kwa taarifa zinadai kuwa kumekuwa na mvutano wa muda mrefu wa kiutendaji baina ya Mbunge Kilufi na Afisa mtendaji huyo Bwna Masweve hali iliyopelekea kuamishwa kwa Afisa mtendaji huyo kutoka Kata ya Mawimbi na kupelekwa kituo cha sasa anachoendelea kufanya kazi cha Kata ya Ruiwa.

CHANZO: mbeya yetu blog
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Gari La Kigogo Chadema Anayekwepa Kodi Ladakwa


Gari lenye namba T 637 ADA aina ya Toyota Land Cruiser, la Coleman Mushi, linalodaiwa kukwepa kulipa kodi tangu Juni 2010, likiwa kituo cha polisi makao makuu Dar es Salaam jana (Ijumaa) mchana kabla ya kurejeshwa kwa mmiliki wake jioni. Picha na mpiga picha wetu.

Na Mwandishi Wetu


GARI la kigogo mmoja anayefanya kazi Mamlaka ya Bandari Tanzania (THA), Coleman Mushi, linalodaiwa kukwepa kulipa kodi, limetiwa mbaroni na polisi.


Habari zilizonaswa zimebainisha kuwa kigogo huyo ambaye ni mfuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alikamatwa maeneo ya Salender Bridge juzi (Alhamisi) usiku.


Gari hilo lilikamatwa kutokana na mtego wa polisi wa usalama barabarani kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) waliodokezwa hila la kigogo huyo kwa barua ambayo nakala yake ilipelekwa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Said Mwema.


Kwa mujibu wa barua ya Oktoba 4 mwaka huu, iliyoandikwa na mkazi wa Dar es Salaam, George Joseph kwenda kwa Kamishna Upelelezi wa Kodi - TRA, gari hilo lenye namba T 637 ADA aina ya Toyota Land Cruiser, linadaiwa kukwepa kulipiwa kodi tangu Juni 2010.


Barua hiyo ilieleza kuwa mmiliki wake hajawahi kulipa kodi ya leseni ya kuliruhusu kutembea barabarani na amekuwa akiliendesha kila siku huku kutoka Gongo la Mboto akapoishi kwenda maeneo mbalimbali Dar es Salaam, akidai yeye ni Ofisa wa Usalama wa Taifa.


Kwa mantiki hiyo, amekuwa akiikosesha mapato Serikali kwa vile gari hilo licha ya kutokuwa na kibali cha kutembea barabarani, pia halina bima na hata mmiliki hana leseni ya kuendesha gari.


Mtego uliowekwa juzi ulimnasa Mushi. . . .
Kwa maelezo zaidi tembeleawww.kwanzajamii.com

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»