Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal kushoto, akizungumza na Mama Maria Nyerere wakati wa Chakula cha mchana kilichoandaliwa na Familia ya Baba wa Taifa Hayati Malimu Julius Nyerere baada ya kumalizika misa maalum kwa ajili ya kumkumbuka Baba wa Taifa pamoja na uwashaji mwenge wa Uhuru iliyofanyika katika kijiji cha Butiama jana. Katikati katibu wa Organaizeshen ya CCM Asha Abdalla Juma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Mama Maria Nyerere katikati, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa ujumbe uliomuwakilisha Rais Yower Museven wa Uganda kwenye Misa maalum ya kumkumbuka Baba wa Taifa Hayati Mwalim Julius Nyerere iliyofanyika jana kijijini kwake Mwitongo Butiama.
Mbunge wa Musoma vijijini Mhe. Nimrold Mkono akijumuika na wasanii wa ngoma ya asili ya mkoa wa Mara kucheza ngoma hiyo, wakati wa sherehe ya kuwasha mwenge iliyofanyika jana katika kijiji cha Butiama mkoani Mara jana.
Vijana wa Halaiki kutoka Shule za mikoa mbalimbali ya Tanzania wakifanya Halaiki ya onesho la kijeshi wakati wa sherehe ya kuwasha mwenge iliyofanyika jana katika kijiji cha Butiama mkoani Mara. Picha na Amour Nassor VPO.
[ Read More ]
Posted by newstz.blogspot.com
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Mwenge wa uhuru kiongozi wa mbia za mwenge huo mwaka 2011 2012 Mtumwa Rashid Halfan kutoka mkoa wa kaskazini Unguja, kwa ajili ya kuanza mbio za kukimbiza katika mikoa yote ua Tanzania baada ya kuuwasha rasmi leo katika kijiji cha Butiama Mkoani Mara.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka shada la mauwa kwenye Kaburi la Hayati Baba wa Taifa Mwalim Julius Nyerere baada ya misa maalum ya kumkumbuka muasisi huyo Taifa la Tanzania iliyofanyika leo kijijini kwake Mwitongo Butiama.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzinduwa kanuni za sheria ya Filamu na Michezo ya kuigiza iliyoambatana na maadhimisho ya miaka 50 Uhuru wa Tanzania Bara zilizofanyika jana katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mara. Kulia Waziri wa Habari utamaduni na Michezo Mhe. Dkt Emanuel Nchimbi na kushoto ni Naibu waziri katika wizara hiyo Dkt Fenella Mukangara
Mwandishi wa Habari na mpiga picha mwandamizi wa Idara ya Habari Maelezo Bi. Anna Itenda, kwa niaba ya waandishi wa habari wa Tanzania, akiweka shada la mauwa katika kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalim Julius Nyerere wakati wa misa maalum ya kumkumbuka muasisi wa Taifa la Tanzania iliyofanyika jana kijijini Mwintongo Butiama.
[ Read More ]
Posted by newstz.blogspot.com