Showing posts with label ajali iringa. Show all posts
Showing posts with label ajali iringa. Show all posts

SUMRY YAGONGANA NA LANDCRUISER YA DKT WA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA NA KUSABISHA KIFO NJE KIDOGO YA MKOA WA IRINGA








Picha mbalimbali za ajali mbaya iliyotokea jana katika sehemu ya Mtandika, mbele kidogo ya hoteli maarafufu ya Al Jazeera, mkoani Iringa, iliyohusisha basi la Sumry na gari aina ya Prado iliyokuwa ikiendeshwa na daktari bingwa wa macho katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya. Katika ajali hiyo daktari huyo alifariki papo hapo (kama inayoonekana katika picha), Na katika basi hakuna aliyepoteza maisha licha ya majeraha madogo madogo. Dereva wa basi alikimbia baada ya ajali hiyo na hivi sasa anatafutwa na jeshi la polisi. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi ambapo dereva wa basi alikuwa akijaribu kulipita lori (ku-overtake) katika kona na kukutana uso kwa uso na gari hiyo ya Prado ambayo pia ilikuwa kasi sana.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

AJALI MBAYA YADAIWA KUUA MMOJA IRINGA



Wasamaria wema wakisaidia kumtoa dereva wa daladala baada ya ajali


Lori lililosababisha ajali eneo la Mwangata mjini Iringa mchana huu


Na francis Godwin
Dadaldala lagongana na lori katika eneo la kona za Mwangata katika manispaa ya Iringa majira ya 8 mchana na kuna taarifa kuwa mtu mmoja kufariki dunia katika ajali hiyo mbaya.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wameuambia mtandao huu kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa Lori lenye namba za usajili T164 BDB kupita upande ambao si wake hivyo kulazimika kulivaa daladala hilo ambalo lilikuwa likishuka mteremko wa Mwangata na lori hilo likipanda mlima.
Walisema kuwa kutokana na kona hizo abiria waliokuwa katika daladala walijikuta wakikutana uso kwa uso na lori hilo.
Hata hivyo walisema zaidi ya abiria watano ndio walijeruhiwa vibaya akiwemo dereva wa daladala yenye namba T 229 BGP anayefahamika kwa jina la kazi la Kizibo.
Majeruhi wote wa ajali hiyo wamekimbizwa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa matibabu zaidi huku dereva wa lori hilo amekimbia baada ya kusababisha ajali hiyo.
Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Iringa (RTO) Kedmund Mnubi amethibitisha kutokea kwa ajili hiyo japo taarifa zaidi juu ya tukio hilo ameahidi kuzitoa hivi punde.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»