Showing posts with label jerry muro. Show all posts
Showing posts with label jerry muro. Show all posts

Hukumu kesi ya Jerry Muro mwisho wa mwezi


Hatma ya kesi ya kula njama wala kuomba rushwa ya Sh. milioni 10, pamoja na kujifanya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inayomkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Jerry Murro (30) na wenzake itajulikana Novemba 30, mwaka huu kama washtakiwa wataachiwa huru ama kwenda jela.
Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Frank Moshi ambapo aliyesikiliza kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam na kusema kuwa hukumu ya kesi hiyo itasomwa Novemba 30, mwaka huu mahakamani hapo.
“Kesi hii ilipangwa kutajwa leo, lakini mahakama hii inasema itasoma hukumu dhidi ya washtakiwa mwisho wa mwezi ujao,” alisema Hakimu Moshi.
Mbali na Muro, washtakiwa wengine ni, Edmund Kapama maarufu kama Dokta na Deogratias Mgasa ama Mussa.
Awali, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Januari 28, mwaka huu jijini Dar es Salaam, washtakiwa wote na wengine ambao hawapo mahakamani kwa pamoja wanadaiwa kula njama ya kutenda kosa la kuomba rushwa .
Katika shitaka la pili, ilidaiwa kuwa Januari 29, mwaka huu katika Hoteli ya Sea Cliff, jijini walitenda kosa la kuomba rushwa ya Sh. 10,000,000 kutoka kwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Wage.
Ilidaiwa kuwa washtakiwa waliomba rushwa hiyo baada ya kumtishia Wage kwamba habari zake za ubadhilifu wa fedha za umma kama mhasibu wa halmashauri hiyo zitatangazwa kwenye luninga.
Katika shitaka la tatu, ilidaiwa kuwa Januari 29, mwaka huu katika hoteli ya Sea Cliff, mshtakiwa wa pili na wa tatu wakiwa na nia ovu walijitambulisha kwa Wage kwamba ni watumishi wa umma na maofisa wa Takukuru huku wakijua sio kweli.
Washtakiwa wote kwa nyakati tofauti walikana mashitaka yao na wako nje kwa dhamana.
CHANZO: NIPASHE
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Wakili ‘Amsafisha’ Jerry Muro



Na Happiness Katabazi


WAKILI wa aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Jerry Murro anayekabiliwa na kesi ya kula njama na kuomba rushwa ya sh milioni 10, Richard Rweyongeza ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,imwachilie huru mshtakiwa huyo kwasababu hana hatia katika kesi hiyo inayomkabili.

Wakili Rweyongeza aliwasilisha maombi hayo mahakamani hapo kwa njia ya maandishi nakala yake (gazeti hili inayo) kufuatia amri iliyotolewa na Hakimu Mkazi Frank Moshi aliyoitoa Oktoba mwaka huu ambapo alizitaka pande zote mbili kuwasilisha majumuisho yao kuwaona washtakiwa wana hatia au la kwa njia ya maandishi ambapo upande wa Jamhuri utawasilisha majumuisho yao kesho.

Wakili Rweyongeza alidai kuwa alisikilizwa kwa makini ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa Jamhuri lakini hajasikia kitu chochote kinacho muunganisha Murro na washtakiwa wengine wasiojulikana kula njama kutenda kosa hilo kama shtaka la kwanza kwanza linavyodai kuwa Murro na washtakiwa wenzake ambao ni Deo Mugassa na Edmund Kapama na watu wengine wasiyofahamika walitenda kusa la kushawishi ili wapewe rushwa Sh milioni 10 toka kwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Wage Karoli , Januari 20 mwaka 2010 ili asiwe kurusha tuhuma zake za ubadhilifu wa fedha za umma katika kipindi cha Usiku wa Habari kinachorushwa na Televisheni ya TBC1.

“Shtaka la kwanza katika hati ya mashtaka, linasomeka kuwa kosa lilitendeka Januari 28 mwaka 2010.Lakini ushahidi ulitolewa na Jamhuri ulionyesha kosa lilitendekea Januari 29 mwaka 2010…na hadi mapema Oktoba mwaka huu washtakiwa walimaliza kujitetea na hivyo kesi upande wa utetezi ikawa imefungwa , hati ya mashtaka ilikuwa ikisomeka Murro alitenda kosa hilo Januari 28 mwaka 2010 ndipo upande wa Jamhuri siku hiyo kabla ya utetezi kufunga kesi yao ukaamua kubadilisha hati ya mashtaka na mahakama ilikubali hati hiyo kubadilishwa kutokana na utofauti uliopo kati ushahidi na maelezo yaliyokuwa yameandikwa kwenye hati ya mashtaka.

“Kwa hali hiyo naona upande Jamhuri hauna maelezo ya uhakika yanayoonyesha mteja wangu alitenda makosa hayo na badala yake ikaamua kuleta ushahidi wa kuungaunga na matokeo yake ndiyo maana Murro aliyakana mashtaka yote yanayomkabili mahakamani hapa”alidai Rweyongeza.

Alidai kuwa kesi ya Jamhuri imesimama na kutegemea ushahidi wa shahidi wa tatu (Michael Wage) jambo linawapotosha kwa sisi upande wa utetezi tunamuona Wage siyo shahidi wa kuaminika na wanaoimba mahakama iupuuze ushahidi wake.

Wakili Rweyongeza alidai kuwa katika ushahidi mashahidi wa Jamhuri walidai kuwa shahidi wa tatu(Wage) kwakuanzia aliwapatia washtakiwa wote rushwa ya Sh 9,000,000 katika sehemu ya rushwa ya Sh milioni 10 aliyokuwa ameombwa na washtakiwa, na wakili huyo akadai kuwa kama hivyo ndivyo ni kwanini polisi wasingesubiri Murro apokee rushwa hiyo ndiyo wakamkamate na kuongeza ni kwanini polisi ilifanya haraka kumkamata Murro wakati bado hajapokea rushwa hiyo ya Sh milioni?

“Tunaomba mahakama hii imwachilie huru Murro kwasababu upande wa Jamhuri umeshindwa kuthibitisha kesi yao bila kuacha mashaka yoyote hivyo namalizia kwa kuiomba mahakama hii imuone Murro hana hatia”alidai Rweyengeza.

Februali 15 mwaka 2010, ilidaiwa mahakamani na upande wa Jamhuri kuwa washtakiwa wote walitenda makosa ya kula njama, kushawishi kupewa rushwa ya Sh milioni 10 kutoka kwa Wage na kujipachika kuwa wao ni wa Maofisa ya TAKUKURU.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»