Kenya yatoa uzoefu kwa Bunge la Katiba

Ujumbe maalum kutoka nchini Kenya umehutubia wajumbe wa Bunge la Katiba nchini Tanzania kuelezea uzoefu wao kuhusu mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya nchini Kenya ulivyofanyika.
Akizungumza na Wajumbe wa Bunge maalum la katiba, Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Kenya,Amos Wako ameainisha masuala ya msingi ya kuzingatia katika upatikanaji wa Katiba mpya ya Tanzania.
Bwana Wako ameeleza uzoefu wake wa upatikanaji wa katiba ikizingatiwa kuwa wakati mchakato wa kupata katiba mpya nchini Kenya alikuwa miongoni mwa watendaji wakuuu wa mchakato huo akiwa mwanasheria mkuu wa serikali. soma zaidi

Categories: