Showing posts with label igunga. Show all posts
Showing posts with label igunga. Show all posts

Mkuu wa Shule achomwa moto Igunga

*Adaiwa kuiba saruji ya shule

Na Mwandishi Wetu, Igunga

MKUU wa Shule ya Sekondari ya Mwashiku, Wilaya ya Igunga, Mkoa wa Tabora, Bw. Charles Medadi (42) amepigwa hadi kufa kisha mwili wake kuchomwa moto na wananchi
wenye hasira baada ya kukamatwa akiwa na mifuko minane ya saruji za shule hiyo.

Habari kutoka eneo la tukio zilidaiwa kuwa marehemu alikamatwa na wananchi akiwa na saruji hiyo huku akidaiwa kujiandaa kwenda kuiuza.

"Nilipofika, wananchi walisema Mwalimu huyo alikamatwa akijiandaa kuuza hiyo simenti (saruji). Kumekuwa na malalamiko kuwa vifaa vya ujenzi na fedha shule hiyo vinaibwa na kutumika vibaya, walikuwa wanafuatilia," alisema mtoa habari wetu kutoka eneo la tukio.

Polisi wilayani Igunga ilithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa taarifa zaidi itatolewa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Bw. Antony Rutta kama utaratibu wa jeshi hilo unavyoelekeza.

Wakati tunakwenda mtamboni gari la polisi yenye namba PT 1825 ikiwa na askari saba wakiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai Wilaya ya Igunga, Bw. William Mlekwa, iliwasili mjini hapa ikiwa na mwili wa marehemu huku ukiwa umeungua vibaya.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga. Wakati huo huo Bw. Bathlomeo Charles, (28) mkazi wa Igunga mjini amekatwa mapanga wakati akitoka dukani kwake mjini hapa.

Tukio hilo lilitokea saa 5 usiku wa kuamkia jana eneo la Posta muda mfupi baada ya kufunga dukani lake na kuelekea nyumbani ndipo walipoibuka kundi la watu na kumwamuru kutoa fedha.

Akizungumza kwa taabu akiwa wodi namba 8 katika hospitali ya Wilaya ya Igunga alikolazwa Bw. Charles alisema baada ya kukataa kutii amri ya kutoa fedha watu ahao walianza kumshambuliwa na kumkata kichwani na mkono wa kushoto ambao ulibaki ukining'inia.

Polisi walithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba Kamanda Rutta anatarajiwa kulitolea ufafanuzi zaidi baada ya uchunguzi kukamilika.

CHanzo Majira
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

CCM wakiri hawakustahili ushindi


NAPE ASEMA WAMEPENYA TUNDU LA SINDANO



Na Efracia masaweCHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimekiri kuwa hakikustahili kushinda katika uchaguzi mdogo uliomalizika jimboni Igunga mwanzoni mwa mwezi huu.

Badala yake, kilisema waliopaswa kushinda ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kilikuwa kinaungwa mkono na wananchi wengi.
Hata hivyo, CCM imedai kwamba ushindi wake Igunga umetokana na CHADEMA kutumia vitisho, ikiwamo kumkamata na kumwadhibu Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatuma Kimario, aliyekutwa anakula njama za ushindi wa CCM.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, katika mkutano wa mapokezi ya mbunge aliyechaguliwa, Dk. Peter Kafumu, katika viwanja vya Bakhresa, Manzese, Dar es Salaam.
Dk. Kafumu alishinda kwa tiketi ya CCM kwa kura 26,484 dhidi ya 23,260 za mgombea wa CHADEMA, Joseph Kashindye. Vyama vingine sita, kikiwamo CUF, vilipata kura chache sana ambazo katika jumla yake hazifiki hata 2,800.
Nape alisema: “Kama CHADEMA wasingejihusisha na vitendo vya kikatili, basi leo hii chama hicho kingekuwa madarakani. Nakiri wazi kuwa CHADEMA wangeweza kuchukua kura zaidi ya 5,000 Igunga…
“Tumeshinda kupitia tundu la sindano, hiyo ipo wazi kabisa… CHADEMA waliwateka wananchi kwa asilimia zote. Kosa lao la kwanza waliwakashifu siku moja kabla ya kupiga kura kwa kuwaleta wasomi ili waje wahesabu kura kwa usahihi, hapo ndipo tatizo lilianza.”
Alisema CHADEMA ilikuwa imewateka wananchi wa Igunga, lakini baadaye walikerwa na kitendo cha chama hicho kuingiza walinzi wa kura kutoka nje ya jimbo.
“Nawahakikishieni baadhi ya wanachama waliokerwa na kitendo hicho cha kutokuaminiwa, kiliwafanya kundi kubwa la wanachama hewa wakichague chama cha CCM, tukaongezewa kura, ” alisema Nauye.
Naye Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Kafumu alitumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wote waliomchagua na akaahidi kuwa nao bega kwa bega katika ufanisi wa kazi.
“Nitawatumikia bila ubaguzi wa chama au mtu yeyote. Nawashukuru kwa kila jambo na Mungu awabariki katika shughuli zenu; naomba tuendelee kushikamana,” alisema Kafumu
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

KATUNI: IGUNGA na NATHAN MPANGALA

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»