Showing posts with label viongozi. Show all posts
Showing posts with label viongozi. Show all posts

VIONGOZI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA PAMOJA NA VYOMBO VYA HABARI KATIKA KUTOA TAARIFA MUHIMU.



NA SALAMA NJANI-BEIJING CHINA       

Viongozi wa mataifa mbali mbali duniani wametakiwa kuwa tayari kufanya kazi kwa pamoja na vyombo vya habari hasa katika kutoa taarifa muhimu zinazohusu jamii,siasa,utamaduni na uchumi.

Hayo yameelezwa leo na Rais wa China Central Television (CCTV) Ling Ju wakati wa mkutano wa kwanza wa kimataifa kwa vyombo vya habari na watumiaji wa vyombo vya habari uliofanyika katika ukumbi wa Media Centre Hotel uliopo mjini Beijing China.

Amesema kuwa vyombo vya habari vinawajibika kubeba jukumu la kutangaza kwa kina taarifa zinazohusu maisha ya watu ya kila siku, ikiwemo mafanikio na changamoto zinazoukabili uchumi wa dunia.

Ling Ju amesema watu wote duniani wanategemea vyombo vya habari kama ni mhimili mkuu,kujua hali ya kupanda na kushuka kwa uchumi kwa kina, ili kubuni mbinu mpya za kupambana na maisha.

 Amefahamisha kuwa masuala ya siasa,jamii,utamaduni na uchumi duniani, yanachukua nafasi kubwa katika maisha ya kila siku ya  mwanadamu, hivyo ni jukumu la vyombo vya habari kuhakikisha vinafanya kazi yakukuza uelewa wa watu kuhusu mambo hayo muhimu.

 Amesisitiza kuwa mashirikiano na nguvu ya kutosha kutoka kwa viongozi yanahitajika,pamoja na uhuru wa kutoa taarifa muhimu zikiwemo za uchumi,ambapo kwa sasa vyombo vya habari vinakabiliwa na changamoto sugu ya kutokuwa na uhuru wa kufanya kazi zao ipasavyo.

 Amesema hakuna chombo chochote cha habari kinachoweza kufanya kazi na kufanikiwa peke yake bila ya mashirikiano ya viongozi wa nchi husika, wanajamii ambao ni walengwa pamoja na vyombo vyengine vya habari vya kimataifa.

 Akizungumzia mafaninikio ya CCTV tokea kuanzishwa kwake mwaka 1958 amesema kupitia vituo na chanel zake mbali mbali imefanikiwa kuunganisha nchi nyingi duniani zikiwemo za Afrika katika kutoa habari muhimu kwa jamii sambamba na matumizi ya teknolojia mpya za kupata habari.

Katika mkutano huo ambao unazishirikisha nchi zaidi ya thelathini ni wa kwanza kufanyika, ikiwa ni mikakati ya kuweka mashirikiano ya nchi nyingi duniani kihabari pamoja na kujua umuhimu wa jamii katika upashaji wa habari.
            
 IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 20/10/2011
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Mwinyi-Viongozi wa dini mnanuka




RAIS mstaafu Ali Hassan Mwinyi, amesema viongozi wa dini kutoka Tanzania wanatia aibu na kuchangia Watanzania kunuka nje ya nchi kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya.

Mzee Mwinyi alitoa kauli hiyo jana mbele ya viongozi hao na kusimulia mkasa uliomkuta yeye binafsi wa kupekuliwa kupita kiasi katika kiwanja cha ndege nje ya nchi, akishukiwa kuwa kiongozi wa dini kutoka Tanzania anayesafirisha dawa za kulevya.


Alikuwa akizindua Baraza la Viongozi wa Dini la Kupambana na Athari za Dawa za Kulevya jana Dar es Salaam katika hafla iliyoandaliwa na asasi ya kiraia ya American International Health Alliance (AIHA).

“Ninachokisema kuna maneno mengi ya aibu yanasemwa kuhusu Watanzania, aibu zaidi hata kwa wacha Mungu wa Tanzania sasa hawaaminiki, wanatumia fursa walizonazo kuficha na kusafirisha dawa za kulevya.

“Nilikuwa naenda Ujerumani hivyo nililazimika kubadili ndege katika moja ya nchi huko ughaibuni, wakati wa kupanda ndege ya pili tukaanza kukaguliwa. Ilipofika zamu yangu, nilikaguliwa sana, lakini hawakutosheka, nikaingizwa kwenye chumba cha pembeni, nikavuliwa viatu na koti wakanikagua kwa mashine na mwisho wakanipapasa mwili mzima,” alisema Mzee Mwinyi.

Alisema alikumbana na kadhia hiyo pamoja na hadhi yake ya kidiplomasia kwa vile tu alikuwa ameshikilia tasbihi (rozari) mkononi, jambo lililofanya ahisiwe kuwa ni kiongozi wa dini anayesafirisha dawa za kulevya.

“Yule aliyenikagua alikuwa akifanya kazi yake, amenifundisha, lakini nataka mjue Watanzania wenzangu kuwa tunanuka huko nje,” alisema Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa wakati wa utawala wake.

Mzee Mwinyi alilazimika kutoa mkasa huo uliompata miaka mingi iliyopita bila kutaja mwaka wala uwanja husika mbele ya viongozi hao wa dini mbalimbali ili kufikisha ujumbe kwao kuwa Tanzania inanuka kwa kuhusishwa na dawa za kulevya.

Alisema mmoja wa wasaidizi wake alijaribu kumnusuru katika hali hiyo kwa kumtahadharisha ofisa wa uwanja huo wa ndege kuwa huyo anayemkagua ni mwanadiplomasia.

“Lakini bwana yule alimjibu tena kwa ukali ‘I don’t care’ (sijali), wakaendelea kunikagua wanavyotaka baadaye nikajiuliza kwani imekuaje wakanikagua vile, nikagundua kuwa ni kwa vile nimebeba tasbihi,” alisimulia Mzee Mwinyi.

Alisema alionekana kama mwanadini anayetumia alama ya tasbihi ili apitishe dawa za kulevya kirahisi, jambo ambalo lilimsikitisha na wakati anaondoka uwanjani hapo, alilazimika kumkabidhi yule ofisa aliyemkagua tasbihi yake kama zawadi.

Kauli hiyo ya Mzee Mwinyi, imetolewa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwataka viongozi wa dini kukemea uhalifu huo na kutahadharisha kuwa sasa biashara hiyo imeaanza kuvutia viongozi wa dini.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo alipokuwa akiwahutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga, kwenye ibada maalumu ya kupewa kuwekwa wakfu Mhashamu Askofu John Ndimbo wa Jimbo hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema Serikali imejipanga kuhakikisha kunakuwa na sheria moja yenye nguvu itakayoziba mianya yote inayojitokeza katika sheria za dawa za kulevya.

Alisema kwa sasa sheria zilizopo zina mianya mikubwa ambayo inasababisha mapapa wa biashara hiyo na vipapa vidogo vinavyokamatwa kuishia kulipishwa faini ya Sh. milioni moja na kutoka.

“Sheria inasema wazi ukikamatwa na dawa za kulevya unalipishwa mara tatu ya gharama ya mzigo wa dawa hizo, kifungo cha miaka 30 au maisha lakini hivi kweli mmeshawaona watu wakifungwa kwa kosa hilo, lazima kuwe na marekebisho katika sheria hizi,” alisema

Kamishna wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Christopher Shekiondo, alisema kikosi kazi maalumu kilichopo chini ya Tume hiyo kimekamata watu wengi wanaotuhumiwa kufanya biashara hiyo.

Takwimu zinaonesha mwaka 2008 hadi mwaka huu, watuhumiwa 22,814 walikamatwa nchini na 67 nje ya nchi huku idadi ya dawa zilizokamatwa ikiongezeka.

Kwa mujibu wa Shekiondo, dawa zilizokamatwa zimeongezeka kutoka heroine kilo 100 kutoka mwaka 2000 hadi 2009 hadi kilo 154 mwaka jana na mwaka huu; na cocaine kilo 57 mwaka 2000 hadi 2009 hadi kufikia kilo 191 mwaka 2010 hadi mwaka huu.

Baraza hilo la Viongozi wa Dini kazi yake ni kuhamasisha vijana kuepuka biashara na matumizi ya dawa za kulevya na linaongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum.

Chanzo: HabariLeo
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MAlUMBANO YASABABISHA UKWASI WA MAENDELEO WILAYANI MBARALI.


Daraja la Kijiji cha Ijumbi, kata ya Ruiwa wilayani Mbarali mkoani Mbeya, ambalo hutumiwa na wananchi kuvuka kuelekea kijiji jirani, ambapo wananchi wengi wamekuwa wakifa kutokana na kuteleza. Mradi wa TASAF ulitoa msaada wa ujenzi wa daraja la uhakika lakini mpaka sasa kumekuwa na marumbano baina ya uongozi waHalmashauri ya mbarali, Kata husika na wananchi ya kwamba ni sehemu gani sahihi lapaswa kujengwa.
Serikali ngazi ya Mkoa ingilieni suala hili ili kunusuru madhara ya kifo kutokana na daraja hili marumbano mpaka lini.

Kwa tafti iliyofanywa na mtandao huu (mbeya yetu) umebaini kuwepo kwa marubano baina ya viongozi wa serikali ya kata, vijiji na wananchi, katika meneo ya kijiji cha Kanioga, Ijumbi, Nsonyanga, Mapogolo, Kapunga na Mawindi. Ambapo baadhi ya watendaji hutafuna fedha za miradi lakini hatua za kisheria hazichukuliwi dhidi yao
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

UZINDUZI WA BARAZA LA VIONGOZI WA DINI LA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA KUFANYIKA OKTOBA 11

Viongozi wa Dini Mbalimbali wakiwa katika picha pamoja na Waratibu kutoka TUME,Wizara ya Afya,Taasisi ya AIHA pamoja na Taasisi CDC.



Ili kukabiliana na matumizi haramu ya dawa za kulevya, Tume ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeratibu uanzishwaji wa Baraza la Viongozi wa Dini la Kupambana na Dawa za Kulevya.

Baraza hili linaundwa na wajumbe Kumi na nne,wajumbe saba kutoka katika taasisi za Kikiristo na wajumbe saba kutoka katika taasisi za Kiislamu.

Jukumu la Baraza hili litakuwa ni kusimamia utoaji wa huduma za kiroho kwa watumiaji wa dawa za kulevya wanaopata nafuu na kutoa elimu kwa vijana kuhusiana na kujikinga na matumizi haramu ya dawa za kulevya katika taasisi zao na jamii yote kwa ujumla.

Uanzishwaji wa Baraza hili umefadhiliwa na Serikali ya watu wa Marekani Kupitia Centers for Disease Control and Prevention (CDC) pamoja na taasisi ya American International Health Alliance (AIHA).

Baraza hilo litazinduliwa Rasmi tarehe 11 Oktoba mwaka 2011, katika hoteli ya Hilton Double Tree, Masaki, Dar es Salaam kuanzia saa tatu na nusu asubuhi.Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo atakuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mheshimiwa Ally Hassan Mwinyi.

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Tibaijuka awatangazia kihama Viongozi Halmashauri

Na Godfrey Ismaely (Majira)

WAZIRI wa Aridhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Ana Tibaijuka, ametangaza kihama dhidi ya viongozi wa Halmashauri zote zilizikopeshwa fedha kwa ajili ya
kupima viwanja na kushindwa kuzirejesha.

Mbali na hilo pia waziri Tibaijuka, awaagiza wote wanaoendeleza ufugaji mijini wajiandae kuondoa mifugo hiyo mara moja kwa kuwa sheria ya mipango miji namba nane ya mwaka 2007 inazuia shughuli hiyo mijini.

Akizungumza Dar es Salaam jana katika maadhimisho ya siku ya makazi Duniani, Waziri Tibaijuka alisema hawezi kuendelea kukaa kimya huku shughuli zilizoainishwa kisheria na kuridhiwa na wabunge zikisimama kwa uzembe wa watendaji wachache.

"Ukimya wa muda mrefu unatufanya tushindwe kuyafikia malengo yetu, kuanzia leo na kuendelea Halmashauri zote ambazo zilikopeshwa fedha na Wizara ili kupima viwanja kwa ajili ya kuviuza ama kuvigawa kwa wananchi zisiporejesha madeni hayo zikae tayari, kihama kimekaribia na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watendaji," alisema Profesa Tibaijuka.

Alisema kushindwa kwa halmashauri hizo kurejesha fedha hizo kunachangia utegemezi nyingine ambazo zilikuwa zinategemea fedha hizo kushindwa kupima viwanja hivyo ubadhirifu na hata tabia za kujimilikisha viwanja visivyopimwa kuendelea kila siku.

"Haiwezekani Halmashauri kukopeshwa fedha ili kupimia viwanja na baada ya kupima na kuviuza kushindwa kurejesha fedha hizo, hapa tutakuwa tunachokozana kwa kuwa halmashauri zingine zitashindwa kuendesha zoezi.

Kilichobakia kwa mtu anayekuchokoza ni vyema ukamchukulia hatua za kisheria, toka mwaka 2008 Wizara ilizikopesha Halmashauri za Manispaa ya Ilala, Temeke na Kinondoni zaidi ya sh. bilioni 1.4 ili kupimia viwanja ili nalo tutalifanyia kazi," alisema Profes Tibaijuka.

Akizungumzia ufugaji mijini unaoendelea alisema sheria ya nchi hairuhusu kufanya hivyo badala yake kwa muda mrefu walivumilia lakini kutokana na ukuaji wa miji tayari wizara inataka ufugaji huo usitishwe mara moja.

"Sheria hairuhusu kufuga mifugo mijini badala yake kama mtu ana shauku ya kufuga kabla ya kihama kumpitia ni vyema akaelekeza jitihada hizo vijijini kwa kuwa mijini kilichobakia ni kusimamia upangaji wa mipango miji na kuisimamia.

Kama watu watalipuuzia tamko hili basi wasinilaumu wakati nikitekeleza kile kilichoainishwa katika sheria ili kuweka miji yetu iwe safi," alisisitiza.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»