KAMATI YA BUNGE YA FEDHA NA UCHUMI YAFANYA ZIARA MKOANI TANGA


Mwengekiti wa kamati ya bunge ya fedha na uchumi,Abdala Kigodo (katikati) akieleza jambo kwenye ofisi ya TRA Tanga walipofanya ziara mkoani hapo. kulia ni katibu wa kamati,Maiko Kadebe na kushoto ni Kamishina wa forodha,Walid Juma.
Kamati ya bunge ya fedha na uchumi ikichangishana fedha za kusaidia ujenzi wa ofisi ya wajasiliamali walemavu wa viungo wa Mwamboni mkoani Tanga.kutoka kulia ni mwenyekiti wa kamati hiyo,Abdala Kigoda wa pili mjumbe wa kamati hiyo Dr. William Mgimwa na watatu ni Richard Ndassa mjumbe wa kamati hiyo pia.
Mjumbe wa kamati ya bunge ya fedha na uchumi,mbunge wa jimbo la Magogoni Pemba,Kombo Khamis Kombo akiongesha kiatu kilichotengenezwa na kikundi cha wajasiliamali walemavu cha Mwamboni mkoani Tanga.kushoto ni Mwengekiti wa kamati hiyo,Abdala Kigoda na kulia ni mwenyekiti wa walemavu,Ally Shekuwe walipofanya ziara mkoani hapo hivi karibuni.
Mwenyekiti wa kikundi cha wajasiliamali cha Mwamboni mkoani Tanga,Ally Shekuwe kushoto akiteta jambo na mjasiliamali wa bidhaa za viatu Jackson Kingusa baada ya kupokea zaidi ya shs. laki tatu kutoka kwa kamati ya bunge ya fedha na uchumi za kukarabati ofisi hiyo ilipofanya ziara mkoani hapo
Benk ya NMB tawi la Madaraka mkoani Tanga limegawa fimbo 30 zenye thamani ya Shs. laki sita na arobaini kwachama cha walemavu wasioona mkoani Tanga
Kamati ya bunge ya fedha na uchumi ikitoka kuzuru jengo la bandari ya Tanga ikiwa ni sehemu ya ziara yao mkoani humo.
Jeshi la Polisi mkoani Tanga linavyo kabiliana na madereva wa pikipiki maalufu kama bodaboda kwa kubeba abiria wengi kinyume na utaratibu yaani mishikaki .