Yusuf Manji (Picha kutoka Maktaba).
********
Na Zahoro Mlanzi
ALIYEKUWA Mfadhili wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji ametua nchini jana alfajiri akitokea Marekani na kutaka apewe wiki moja atafakari
juu ya kusaini mkataba mpya wa kuifadhili tena timu hiyo.
Hali hiyo imetokana na uongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti, Llody Nchunga kumwandikia barua mfadhili huyo kumuomba arejee Yanga kuokoa jahazi.
Wakati Nchunga akiwaza hilo, wiki iliyopita wachezaji wa timu hiyo ilidaiwa kugomea mazoezi wakishinikiza walipwe mishahara yao wanayoidai klabu hiyo.
Akilithibitishia gazeti hili Dar es Salaam jana juu ya ujio wa Manji, Ofisa Habari wa klabu hiyo Louis Sendeu, alisema kweli ameshatua nchini lakini kwanza anataka kukutana na wazee wa klabu na Kamati ya Utendaj ndipo mengine yafuate.
"Ni kweli amekuja na hajasaini mkataba, ila ametoa wiki moja kwanza aangalie wapi kwa kuanzia maana kuna mambo mengi anataka kufanya kwa sasa.
"Kuna Uwanja wetu wa Kaunda unatakiwa umaliziwe, tuna kiwanja mtaa wa Mafia ambacho tunataka kujenga kitega uchumi, hivyo ukiangalia kiukweli mambo ni mengi," alisema.
Alisema baada ya kukutana na wazee wa klabu pamoja na viongozi na kujadili kwa kina na kufikia muafaka, ndipo atakaposaini mkataba mpya baada ya awali kujiondoa.
Manji alijiondoa katika kuifadhili timu hiyo kutokana na viongozi wa klabu hiyo, kudaiwa kuzitumia vibaya fedha zilizotolewa kwa ajili ya maandalizi ya Kombe la Kagame.
Mbali na fedha hizo, pia ilidaiwa walizitumia vibaya fedha za usajili na hata baadhi ya wachezaji kushindwa kulipwa baadhi ya marupurupu yao.
********
Na Zahoro Mlanzi
ALIYEKUWA Mfadhili wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji ametua nchini jana alfajiri akitokea Marekani na kutaka apewe wiki moja atafakari
juu ya kusaini mkataba mpya wa kuifadhili tena timu hiyo.
Hali hiyo imetokana na uongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti, Llody Nchunga kumwandikia barua mfadhili huyo kumuomba arejee Yanga kuokoa jahazi.
Wakati Nchunga akiwaza hilo, wiki iliyopita wachezaji wa timu hiyo ilidaiwa kugomea mazoezi wakishinikiza walipwe mishahara yao wanayoidai klabu hiyo.
Akilithibitishia gazeti hili Dar es Salaam jana juu ya ujio wa Manji, Ofisa Habari wa klabu hiyo Louis Sendeu, alisema kweli ameshatua nchini lakini kwanza anataka kukutana na wazee wa klabu na Kamati ya Utendaj ndipo mengine yafuate.
"Ni kweli amekuja na hajasaini mkataba, ila ametoa wiki moja kwanza aangalie wapi kwa kuanzia maana kuna mambo mengi anataka kufanya kwa sasa.
"Kuna Uwanja wetu wa Kaunda unatakiwa umaliziwe, tuna kiwanja mtaa wa Mafia ambacho tunataka kujenga kitega uchumi, hivyo ukiangalia kiukweli mambo ni mengi," alisema.
Alisema baada ya kukutana na wazee wa klabu pamoja na viongozi na kujadili kwa kina na kufikia muafaka, ndipo atakaposaini mkataba mpya baada ya awali kujiondoa.
Manji alijiondoa katika kuifadhili timu hiyo kutokana na viongozi wa klabu hiyo, kudaiwa kuzitumia vibaya fedha zilizotolewa kwa ajili ya maandalizi ya Kombe la Kagame.
Mbali na fedha hizo, pia ilidaiwa walizitumia vibaya fedha za usajili na hata baadhi ya wachezaji kushindwa kulipwa baadhi ya marupurupu yao.
Categories:
yanga,
yusuf manji