Showing posts with label yanga. Show all posts
Showing posts with label yanga. Show all posts

KOCHA WA YANGA KOSTADIN PAPIC ATUA JANGWANI KUKINOA KIKOSI HICHO KUCHUKUA NAFASI YA SAM TIMBE


Na Francis Dande

Katika kuhakikisha inashinda katika pambano lake dhidi ya mtani wa jadi Simba, Klabu ya Yanga imemrejesha kocha wake aliyekuwa akikinona kikosi hicho katika msimu uliopika wa Ligi 2010-11 kabla ya kukatisha mkataba wake, Pichani Kocha wa Yanga Kostadin Papic akitoka katika mazoezi ya timu hiyo baada kuifundisha timu hiyo kwa kipindi cha saa moja baada ya kuanza rasmi kazi hiyo akichukua mikoba ya aliyekuwa mtangulizi wake Sam Timbe ambaye mechi yake ya mwisho ilikuwa ya jana kati ya Yanga na JKT Oljoro ambapo yanga iliibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0.

Kocha huyo kutoka Uganda mkataba wake ulikuwa uishe mwezi mei 2012 ambapo alikuwa na jukumu la kuinoa timu hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja, Kocha Papic mtihani wake wa kwanza utakuwa dhidi ya Simba katika mpambanmo utakaofanyika kwenye Uwanja wa taifa Oktoba 29.

Habari za uhakika kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa Sam Timbe tayari ameshapewa barua yake ili kumpisha Kondic. Hata hivyo kabla ya ujio wa Timbe,Papic ndiye aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es Salaam.

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Manji aivutia pumzi Yanga

Yusuf Manji (Picha kutoka Maktaba).


********


Na Zahoro Mlanzi

ALIYEKUWA Mfadhili wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji ametua nchini jana alfajiri akitokea Marekani na kutaka apewe wiki moja atafakari
juu ya kusaini mkataba mpya wa kuifadhili tena timu hiyo.

Hali hiyo imetokana na uongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti, Llody Nchunga kumwandikia barua mfadhili huyo kumuomba arejee Yanga kuokoa jahazi.

Wakati Nchunga akiwaza hilo, wiki iliyopita wachezaji wa timu hiyo ilidaiwa kugomea mazoezi wakishinikiza walipwe mishahara yao wanayoidai klabu hiyo.

Akilithibitishia gazeti hili Dar es Salaam jana juu ya ujio wa Manji, Ofisa Habari wa klabu hiyo Louis Sendeu, alisema kweli ameshatua nchini lakini kwanza anataka kukutana na wazee wa klabu na Kamati ya Utendaj ndipo mengine yafuate.

"Ni kweli amekuja na hajasaini mkataba, ila ametoa wiki moja kwanza aangalie wapi kwa kuanzia maana kuna mambo mengi anataka kufanya kwa sasa.

"Kuna Uwanja wetu wa Kaunda unatakiwa umaliziwe, tuna kiwanja mtaa wa Mafia ambacho tunataka kujenga kitega uchumi, hivyo ukiangalia kiukweli mambo ni mengi," alisema.

Alisema baada ya kukutana na wazee wa klabu pamoja na viongozi na kujadili kwa kina na kufikia muafaka, ndipo atakaposaini mkataba mpya baada ya awali kujiondoa.

Manji alijiondoa katika kuifadhili timu hiyo kutokana na viongozi wa klabu hiyo, kudaiwa kuzitumia vibaya fedha zilizotolewa kwa ajili ya maandalizi ya Kombe la Kagame.

Mbali na fedha hizo, pia ilidaiwa walizitumia vibaya fedha za usajili na hata baadhi ya wachezaji kushindwa kulipwa baadhi ya marupurupu yao.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Msimamo wa VODACOM PREMIER TANZANIA BARA kwa ufupi

Vodacom Ligi:5bora
Timu P Pts
Oljoro 10 19
Simba 8 18
Mtibwa 10 15
Azam FC 8 15
JKT Ruvu 9 15
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

LIGI KUU YA VODACOM-YANGA YAIFUNGA KAGERA SUGAR 1-0 LEO NESHNO


Golikipa wa Kagera Suga, Hannington Kalyesubula akioko moja ya hatari zilizoelekezwa langoni mwake mbele ya beki wa Yanga, Nadir


Yanga wakifurahia ushindi wao
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»