Dar na Zanzibar visiwani kukosa umeme kwa siku kadhaa kufuatia kulipuka kwa transifoma ubungo jioni ya jana


Moja ya Transifoma iliyopo katika Kituo cha Umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam (Ubungo Grid Sub Station) imeungua moto jioni hii. Akizungumza na waandishi wa
 habari katika eneo la tukio, Naibu Mkurugenzi wa Tanesco, Bi. Sophia Mgonja
 amesema kuwa, kutokana na hitilafu hiyo Jiji la Dar es Salaam na Visiwa vya
 Zanzibar vitakosa umeme kwa siku kadhaa. Akifafanua zaidi juu ya tukio hilo, 
Mgonja alisema lilitokea baada ya kifaa cha kurekebisha nguvu ya umeme 
kiitwacho Reactor kuungua. Picha hizi zinawanyonyesha wafanyakazi wa kikosi 
cha zima moto wakizima moto katika Transifoma iliyokuwa ikiungua.
Picha kwa hisani ya Kulwa Mwaibale/Global Publishers .

Categories: ,