Habari Na Mery Ayo,Arusha.
Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo(chadema) Bw Freeman Mboye leo amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi kwa makosa mawili ambayo aliyafanya mjini hapa na kukiuka sheria za nchi
Akisomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa serikali Bw haruna Matagani mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bi Devotha Kamuzora, mtuhumiwa mboye alidaiwa kufanya makosa hayo wakati wa mkutano wa hadhara.
Aidha iliendelea kudaiwa mahakamani hapo kuwa katika kosa la kwanza mtuhumiwa alikuwa ni miongoni mwa watu ambao waliongoza mkutano baada ya muda wa mkutano kuisha jambo ambalo ni kinyume cha sheria na taratibu za jeshi la polisi.
Pia kosa la pili ni pamoja na kukataa kutii amri ya jeshi la polisi ambapo amri hiyo iliwataka kutawanyika kwa ajili ya sababu za kiusalama zaidi jambo ambalo mtuhumiwa huyo alikataa.
‘jeshi la polisi liliwataka wafuasi watawanyike baada ya kumazika kwa mkutanoa ambao ulikuwa na kibali halali lakini haikuwa hivyo badala yake waliendeleza mkutano pamoja na jeshi hilo kuwasihi juu ya kutawanyika hivyo sheria na amri za polisi zilikiukwa” iliongezwa mahakamani hapo.
Kutokana na mashitaka hayo mtuhumiwa huyo alikana mashitaka yote ambayo amesomewa na hivyo kuweza kuahirishwa kwa kesi hiyo mpaka November 22 mwaka huu ambapo itasomwa tena mahakamani hapo na mahakama iliridhia kumuachilia huru mara baada ya kukidhi masharti ya dhamana.
Hata hivyo kwa upande wa washitakiwa hao wanaotetewa na wakili methody kimomogoro ambaye pia ni wakili kwa upande wa watuhumiwa wengine.
Katika hatua nyingine mji wa arusha umeonekana kuwa shwari zaidi baada ya kusitishwa kwa maandamano ambayo yalikuwa yamepangwa kufanyika hali ambayo mpaka sasa inaonekana kuleta amani na utulivu
Categories:
chadema,
Godbless Lema,
mh Freeman Mbowe