Showing posts with label mh Freeman Mbowe. Show all posts
Showing posts with label mh Freeman Mbowe. Show all posts

HAKIMU AKATAA OMBI LA KUKAMATWA MBOWE, LISSU

Habari Na Peter Saramba, Arusha.

MAHAKAMA ya hakimu mkazi Arusha, jana ilikataa kutoa hati ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu lililowasilishwa na upande wa mashtaka baada ya washtakiwa hao kutofika mahakamani.

Hakimu Mkazi, Devotha Msofe alikataa ombi la wakili wa serikali, Haruna Matagane kwa sababu yeye alipaswa kutekeleza jukumu la kuahirisha shauri hilo la jinai namba 454 ya mwaka huu inayowakabili viongozi wa juu, wanachama na mashabiki wa Chadema wanaodaiwa kufanya mikusanyiko isiyo halali kati Saa 12 jioni ya Novemba 7 hadi 8, mwaka huu.

Kwa mara ya kwanza, ilisikilizwa na hakimu Devotha Kamuzora ambaye jana alikuwa na dharura, hivyo mwenzake Msofe kusaidia kutaja na kuiahirisha hadi Desemba 20 mwaka huu itakapotajwa tena ili kupangiwa tarehe ya kusikilizwa baada ya upande wa mashtaka kuieleza mahakama kuwa upelelezi umekamilika.

“Mimi leo nina jukumu moja tu la kuahirisha shauri hili, nadhani ni vema maamuzi ya kutoa hati hiyo kama upande wa mashtaka unavyoomba yakatolewa na hakimu anayesikiliza kesi hii,” alisema Hakimu Msofe.

Kwa upande wake, wakili wa utetezi, Method Kimomogoro alieleza mahakama kuwa wateja wake walishindwa kufika mahakamani jana kutoka na tatizo lililokuwa nje uwezo wao baada ya ndege waliyopanga kusafiria jana asubuhi kubadilisha ratiba ya safari yake.

Wakili huyo aliomba kuwa iwapo ni lazima wawepo mahakamani, basi shauri hilo liahirishwe kwa muda hadi mchana ambapo ndege hiyo ingekuwa imefika kabla ya muda wa mahakama kumalizika saa 9:30 alasiri.

Kimomogoro alidai washtakiwa hao walishindwa kufika Arusha mapema kabla ya jana kwa sababu walikuwa wakihudhuria vikao vya kamati kuu (CC) ya Chadema ambavyo Mbowe ndiye mwenyekiti wake huku Lissu akiwa mjumbe, vikao alivyodai vilimalizika usiku wa kuamkia jana.

Licha ya wakili serikali kupinga hoja hizo za utetezi akidai washtakiwa walipaswa kupanga na kufanya vikao vya mapema kabla ya siku zinazokaribiana na tarehe ya kesi, hakimu Msofe alisema zina msingi na kuhairisha shauri hilo.

Washtakiwa wengine 26 akiwemo Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa walikuwepo mahakamani ambapo wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka matatu tofauti ikiwemo kufanya kusanyiko kinyume cha sheria , kukataa kutii amri halali ya polisi iliyotolewa na kamanda wa oparesheni maalumu mkoa wa Arusha, Peter Mvulla akiwaamuru kutawanyika.

Shtaka la tatu linamkabili Dk Slaa peke yake, anayedaiwa kutoa maneno ya uchochezi Novemba 7 mwaka huu, saa 11.30 jioni kwenye viwanja vya NMC akimtaka IGP Said Mwema kumuhamisha Kamanda wa Polisi Wilaya (OCD) wa Arusha, Zuberi Mwomboje na kuwa watamng’oa Rais madarakani kwa maandamano.

Katika hali iliyozua hofu na wasiwasi kwa wananchi waliohudhuriwa kesi hiyo, idadi kubwa ya askari polisi ilizingira maeneo yanayozunguka mahakama hiyo, huku magari zaidi ya manane ya jeshi hilo, mengi yakiwa na namba za usajili za kiraia yakiwa yameegeshwa kila kona ya viwanja vya mahakama.

Pamoja na idadi kubwa ya polisi, watunisha misulu maarufu kama mabaunsa ambao hawakujulikana mara moja wameletwa na nani walikuwa wakirandaranda kila kona na mara baada ya shauri hilo kuahirishwa walienda kubana pembeni mwa geti la kuingia na kutoka mahakamani bila kujulikana wanavizia kitu gani.

CHANZO: MWANANCHI
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MWENYEKITI WA CHADEMA AFIKISHWA MAHAKAMANI JIJINI ARUSHA LEO


Habari Na Mery Ayo,Arusha.

Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo(chadema) Bw Freeman Mboye leo amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi kwa makosa mawili ambayo aliyafanya mjini hapa na kukiuka sheria za nchi

Akisomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa serikali Bw haruna Matagani mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bi Devotha Kamuzora, mtuhumiwa mboye alidaiwa kufanya makosa hayo wakati wa mkutano wa hadhara.

Aidha iliendelea kudaiwa mahakamani hapo kuwa katika kosa la kwanza mtuhumiwa alikuwa ni miongoni mwa watu ambao waliongoza mkutano baada ya muda wa mkutano kuisha jambo ambalo ni kinyume cha sheria na taratibu za jeshi la polisi.

Pia kosa la pili ni pamoja na kukataa kutii amri ya jeshi la polisi ambapo amri hiyo iliwataka kutawanyika kwa ajili ya sababu za kiusalama zaidi jambo ambalo mtuhumiwa huyo alikataa.

‘jeshi la polisi liliwataka wafuasi watawanyike baada ya kumazika kwa mkutanoa ambao ulikuwa na kibali halali lakini haikuwa hivyo badala yake waliendeleza mkutano pamoja na jeshi hilo kuwasihi juu ya kutawanyika hivyo sheria na amri za polisi zilikiukwa” iliongezwa mahakamani hapo.

Kutokana na mashitaka hayo mtuhumiwa huyo alikana mashitaka yote ambayo amesomewa na hivyo kuweza kuahirishwa kwa kesi hiyo mpaka November 22 mwaka huu ambapo itasomwa tena mahakamani hapo na mahakama iliridhia kumuachilia huru mara baada ya kukidhi masharti ya dhamana.

Hata hivyo kwa upande wa washitakiwa hao wanaotetewa na wakili methody kimomogoro ambaye pia ni wakili kwa upande wa watuhumiwa wengine.

Katika hatua nyingine mji wa arusha umeonekana kuwa shwari zaidi baada ya kusitishwa kwa maandamano ambayo yalikuwa yamepangwa kufanyika hali ambayo mpaka sasa inaonekana kuleta amani na utulivu
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

Mbowe amfuata Lema Magereza

** Amtaka atoke mahabusu kesho ili kuleta utulivu
**JK, Prince Charles wa Ungereza watakuwa Arusha
**Mkutano wa Mnyika waingia dosari, Polisi wavamia

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demekrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, atatoka mahabusu kesho (Jumatatu) na kufanya mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya NMC Ltd.
Mbowe ambaye alifika jijini hapa kumuona Lema katika Gereza la Kisongo, ambako amewekwa mahabusu tangu Jumatatu iliyopita, alisema amemwelekeza atoke kesho.
“Nimekuja hapa kumpa maelekezo Mbunge Lema atoke Jumatatu kwa sababu Jumanne vikao vya Bunge vinaanza na ni muhimu kwake kuhudhuria,” alisema.
Alisema wakati akienda kumuona gerezani, tayari makamishna wawili kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam, pamoja na Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha na Ofisa Upelelezi wa Mkoa wa Arusha, walimtembelea mahabusu kumsihi akubali kutoka ili kuleta utulivu jijini hapa.
Alisema chama chake kimekubali kumwekea dhamana na kumwelekeza atoke mahabusu, kwa sharti walilowapa polisi kwamba baada ya kutoka mahakamani apokelewe na wafuasi wake na kusindikizwa hadi viwanja vya NMC Ltd ambako atazungumza na wapiga kura wake kuelezea yaliyojiri.
Alisema wameamua kufanya hivyo kutokana na vikao vya bunge kuanza Jumanne na kwamba anahitajika kuwepo bungeni.
Awali alisema chama hicho kilipanga kufanya mikutano mikubwa ya hadhara kwa muda wa siku saba kuanzia Jumatatu.
Alisema mikutano hiyo ilipangwa kuanza majira ya saa 4 asubuhi hadi saa 12 jioni, lakini Jeshi la Polisi limewaomba wasitisha kufanya mikutano hiyo kwa sababu katika wiki hiyo kutakuwa na ugeni wa watu mashuhuri jijini hapa.
Alisema polisi walisema ugeni wa kwanza ni ujio wa mtoto wa mfalme wa Uingereza, Prince Charles, ambaye atawasili jijini hapa tarehe 9 na baadaye atakuja Rais Jakaya Kikwete.
Kutokana na ugeni huo, Mbowe alisema polisi wameomba mikutano hiyo isifanyike ili kuleta hali ya utulivu.
Hata hivyo, alisema chama chake kimebeba dhamana hiyo na kuamua kusitisha kwa sharti kwamba Lema aruhusiwe kusindikizwa na wapiga kura wake baada ya kutoka mahakamani hadi kwenye viwanja vya NMC na kuzungumza na wananchi.
Alisema iwapo atazuiwa kufanya hivyo, basi chama chake kitatoa taarifa ya kufanyika kwa mikutano hiyo, licha ya kuwepo kwa ugeni huo.
“Polisi wasijaribu kuzuia wanachama kumpokea Lema wakati akitoka mahakamani Jumatatu wala kuzuia mkutano wake akizungumza na wananchi…mbunge amekaa mahabusu kwa wiki nzima, hivyo alikuwa na ujumbe mzito wa kuueleza umma, ni vema akipewa nafasi ya kuzungumza na wapiga kura wake,” alisema.
Alisema yapo mambo mengi yanayolalamikiwa kama vile suala la umeya, udiwani, manyanyaso ya polisi ambayo watayaeleza katika mkutano huo.
Alisema iwapo polisi watamzuia kufanya mkutano huo, watalazimika kufanya mikutano yao kama kawaida na kwamba ujio wa mtoto wa mfalme utakuwa ni kielelezo kizuri sana cha kupeleka ujumbe kimataifa.
“Mikutano ya siku saba ni maamuzi magumu sana ambayo chama ilifikiria kuchukua, bado ujio wa mtoto wa mfalme kwetu tunauona kuwa ni mzuri wa kupeleka ujumbe, pengine itakuwa ni wakati muafaka kwa dunia kujua yanayotokea Arusha na Tanzania kwa ujumla,” alisema.
MKUTANO WA MNYIKA WAINGIA DOSARI, OPOLISI WAVAMIA
Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni limewakamata watu waliokusanyika kwa ajili ya kumsubiri Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika, kuwahutubia kwa madai ya kuhofia Al Shaabab.
Miongoni mwa waliokamatwa ni pamoja na Diwani wa Sarange, Ephahim Kinyafu, Katibu Mwenezi wa jimbo, Ali Makwiro, mfanyakazi Ofisi ya Mbunge, Julius Mgaya na dereva wa gari ambalo lilikuwa limewekwa kipaza sauti, Jafari Mbaga.
NIPASHE Jumapili jana jioni ilishuhudia purukushani kati ya jeshi la polisi na wafuasi hao ambao walikusanyika eneo la Ubungo karibu na baa ijulikanayo kama Corner baa, kwa lengo la kumsubiri Mbunge wa jimbo hilo.
Wakati wakiendelea kumsubiri, ghafla majira saa 10:27 jioni zaidi ya polisi wanane wakiwa na magari na vitendea kazi mbali mbali walifika eneo hilo na kuanza kuwakamata viongozi hao pamoja na wananchi waliokuwa wamevalia sare za chama hicho.
Hata hivyo, kamata kamata hiyo ambayo ilidumu takriban dakika tano, ilisababisha wafuasi waliokuwepo eneo hilo kuduwaa na kushindwa kufanya chochote dhidi ya polisi hao.
Baada ya askari hao kuwakamata watu hao pamoja na gari lililokuwa limebeba spika, waliondoka eneo hilo na ndipo Mnyika alipowasili eneo hilo na kulazimika kutumia gari lake kama jukwaa kuwahutubia wananchi waliobaki.
Mnyika, aliwaeleza wananchi kuwa, polisi hawajafuata utaratibu.
“Polisi hawajafuata taratibu kwani wanawakamata viongozi waliochaguliwa na wananchi na wanawakataza kuongea na nyinyi kwa kisingizio kuwa kuna Al Shaabab, je swali la kujiuliza hawa Al Shaabab wanafuata nini hapa, nilitegemea wangenikamata mimi,” alisema na kuongeza:
“Ningependa hili la tishio la Al Shaabab ambalo linatumika kama kisingizio Rais atoe tamko, atueleze kuwa nchi ipo kwenye hatari, nakumbuka Jumamosi iliyopita jeshi la polisi hili hili lilizuia maandamano ya wanaharakati waliokuwa wakipinga Dowans na siku hiyo kulikuwa na mpira wa Simba na Yanga na mimi nilikuwa na mkutano Mbezi Msigani na ulifanyika vizuri mbona kisingizio hichi hakikutajwa,” alisema.
Aidha, alisema baada ya mkutano huo ataelekea polisi ili kujua hatma ya waliokamatwa kwa sababu polisi walitakiwa waandike barua kama alivyofanya yeye wakati wa kuomba kufanyika mkutano huo.
Akizungumzia kuhusu lengo la kuitisha mkutano huo, Mnyika alisema lililenga kueleza mafanikio ya jimbo, kukusanya maoni ya katiba ili ayapeleke bungeni.
Pia alisema lengo lingine lilikuwa ni kugawa nyaraka kwa wananchi zilizoelezea suala katiba ambazo hata hivyo mbunge huyo alieleza zimechukuliwa na polisi hao.
Kufuatia tukio hilo, Mnyika aliwaeleza wananchi kuwa, polisi watalazimika kulipa gharama zote ambazo zimetumika kufanikisha mkutano huo.
Katika maoni ya wananchi yaliyotolewa kwenye mkutano huo yalieleza kitendo cha serikali kutowashirikisha kwenye mchakato wa katiba mpya, upanda kwa gharama za maisha na kukataa kulipwa kwa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema wamelazimika kuuvunja mkutano huo kutokana na barua waliyoipokea kutoka kwa mbunge huyo kutojitosheleza baadhi ya mambo pamoja na kuhofia matukio ya kigaidi ambayo yamekuwa tishio nchi mbalimbali duniani.
Kenyela alisema alipokea barua hiyo jana (juzi) huku ndani yake ikionyesha imeandikwa kutoka Alhamis ya wiki hii (Novemba 3).
"Barua hii ya Mnyika iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho,'Maombi ya kushiriki ziara jimbo la Ubungo' ilikuwa na mapungufu kwanza haikutaja tarehe wala siku ya ziara hiyo, zaidi ilibainisha maeneo ya ziara kuwa ni Kibo na Usewe na muda ambao ni kuanzia saa 8:00 mchana hadi saa 12:00 jioni," alisema.
Kenyela alisema kutokana na tatizo hilo kujitokeza kwenye barua hiyo, jana (juzi) alilazimika kumwandikia barua mbunge huyo kumweleza upungufu huo kwenye barua yake.
Alisema barua aliyoiandika kwa Mnyika pamoja na sababu ya kutokuwa na tarehe na muda wa ziara iliyopangwa, pia alimweleza kuwa haikueleza ni ofisi/taasisi zipi ambazo atazizindua na majina ya wahusika wake.
"Hofu yetu sasa hivi ni haya matukio ya ugaidi yanayoendelea duniani, tulifikiri mbunge huyu angetujibu barua tuliyomwandikia badala yake, ameamua kufanya mkutano," alisema.
Hata hivyo, Kenyela hakubainisha idadi ya watu wanaowashikilia kutokana na tukio hilo.
CHANZO: NIPASHE
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MH MBOWE AFANYA ZIARA YA WIKI MBILI JIMBONI KWAKE


Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai Mh Freeman Mbowe akisikiliza maelezo ya mhandisi , Pissy juu ya namna ya kumaliza tatizo la ubovu wa barabara inayoelekea kwenye kituo cha Afya cha Kisiki ambapo Dr mkuu wa kituo hicho ,Isdory Kavishe (mwenye koti jeupe) naye alimshukuru mbunge huyo kwa kuamua kushughulikia tatizo hilo kwa kile alichosema kuwa imekuwa ikipitika kwa shida hasa kipindi cha mvua kutokana na utelezi


Mh. Mbowe akikagua kivuko cha miguu cha Miase nikinachounganisha kitongoji cha Mwara na Mashare ambacho kinahitaji kufanyiwa matengenezo baada ya kingo zake kumomonyoka kutokana na mvua zilizonyesha hizi karibu huku kukiwa na hitaji ya kukibadilisha kukitengeneza kwa kutumia reli.


Mbowe akisikiliza malezo ya mwenyekiti wa kijiji cha Nshara , Awadhi Uronu (aliyekunja mikono) kuaharibika kwa kivuko cha waenda kwa miguu kilichoharibiwa na mvua zilizonyesha hivi karibuni , aliambatana na mwenyekiti wa halmashauri hiyo , Clemence Kwayu (mwenye Kaunda suti nyeusi). Picha na Habari na Grace Macha

******

MWENYEKITI wa Taifa wa CHADEMA Freeman Mbowe yuko kwenye ziara ya wiki mbili jimboni kwake kukagua miundo mbinu ya barabara za vitongoji na vijiji akiwa ameambatana na mhandisi wa halamshauri ya Hai Bw. Cosmas Pissy na wataalamu wengine wa idara hiyo .
Kazi kubwa ilikuwa ni kutathmni maeneo korofi kwa lengo la kuyawekea mkakati maalum wa kuyatengeneza kwa kuainisha aina ya marekebisho yanayohitajika na gharama zake ili ziweze kutengenezwa .
Alipita kukagua barabara inayopita pembeni ya soko la Kalali ambapo wanachi waliacha shughuli zao na kumfuata huku wakimweleza kuwa wanaendelea kutozwa ushuru wa soko wakati ulishafutwa ambapo Mbowe aliahidi kulishughulikia suala hilo kwa kuongea na Mkurugenzi wa halmashauri ili amweleze ni kwa nini wanaendelea kutoza ushuru wakati tayari walishaufuta kupitia kikao cha baraza la madiwani na walikubaliana kuanzia Oktoba mwaka huu usitozwe kwa wale wenye kuuza bidhaa ndogondogo kwenye masoko yote ya wilaya hiyo.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»