CCM yapumulia mashine




•  AJALI YA MV SKAGIT, URAIS 2015

VYAITESA

na Mwandishi wetu

UPEPO wa mabadiliko ya kisiasa

uliozikumba nchi nyingi duniani,

unaelekea kukiathiri Chama Cha

Mapinduzi (CCM) ambacho sasa

kinahaha kujinusuru kung’oka

madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa

mwaka 2015.

Chama tawala hivi sasa kina

msuguano mkubwa wa kiuongozi

ambapo baadhi ya viongozi wake

wamekuwa wakimshutumu Katibu

Mkuu, Willison Mukama, kwa

kukwamisha mikakati ya kujiimarisha

na kurejesha matumiani yaliyofifia

miongoni mwa wanachama wake.

Licha ya Katibu wa Itikadi na Uenezi,

Nape Nnauye, wiki hii kukanusha

kutokuwa na msuguano na Mukama,

makada wa chama hicho

wamelidokeza Tanzania Daima

Jumapili, kuwa vita ya makundi ya

kuwania uongozi na ile ya ufisadi

inakitesa chama hicho.

Mnyukano wa kisiasa unaonekana

wazi hivi sasa ni baina ya Waziri wa

Mambo ya Nje na Ushirikiano wa

Kimataifa, Bernard Membe, dhidi ya

kundi linalomuunga mkono aliyekuwa

Waziri Mkuu, Edward Lowassa,

anayetajwa kutaka kuwania urais

katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka

2015.

Wakati hali ya mambo ikionekana

kutokuwa nzuri ndani ya chama hicho,

nguvu kubwa sasa imehamishiwa

kwenye Bunge kwa lengo la

kuwadhibiti wabunge wa CHADEMA

ambao wanaelezwa kutishia uhai wa

chama hicho.

Makada wa CCM wamedokeza kuwa

wamebaini wabunge wa CHADEMA

mwaka 2005-2010 walilitumia vizuri

Bunge kujenga hoja za msingi ambazo

ziliwasaidia kujijenga na hatimaye

kupata wabunge 22 wa majimbo

kutoka watano.

Waliongeza kuwa kutokana na kubaini

jambo hilo, chama hicho kimeamuap

‘kuzishughulikia’ hoja zinazotolewa na

CHADEMA bila kujali kama zina

masilahi kwa taifa au la.

Inadaiwa kuwa viongozi wa Bunge

nao wamepewa maelekezo ya

kukisaidia chama chao hasa

wanapoona kuna hoja zinazoelekea

kuwapatia umaarufu wabunge wa

CHADEMA.

Tanzania Daima Jumapili,

limedokezwa kuwa pamoja na

maelekezo hayo baadhi ya viongozi

wa Bunge wameonekana kushindwa

kukisaidia chama tawala kwa sababu

ya kutozijua ipasavyo kanuni, hivyo

kutumia ubavu kukataa jambo

linalotolewa na wapinzani, hivyo

kuwaongezea umaarufu.

Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai,

anatuhumiwa kutoa fursa zaidi kwa

wabunge wa CCM kurudia maneno ya

dharau na lugha ya kuudhi dhidi ya

wapinzani.

Kiongozi huyo pia juzi alionesha

‘ukada’ wake pale alipojifanya kukosea

jina la Mbunge wa Viti Maalumu, Rose

Kamili, kwa kumuita Rose Kamili Slaa,

ilhali akijua mbunge huyo

alishatarikiana na Dk. Slaa.

Hata hivyo CCM hivi sasa pia

kinakabiliana na wakati mgumu wa

kushutumiwa kushindwa

kuwachukulia hatua watendaji wake

wanaobainika kufanya uzembe katika

shughuli zao za kila siku.

Ajali ya mv Spice Islanders iliyotokea

mwaka jana na mv Skagit iliyotokea

wiki iliyopita inadaiwa ilichangiwa na

uzembe wa wataalamu kwa

kushindwa kukagua ubora wake.

Serikali ya CCM pia inalaumiwa kwa

kushindwa kuwa na vifaa vya kisasa

vya uokoaji licha ya kila mara

kukumbwa na matukio ya ajali za

baharini na ziwani.

Katika ajali hizo mbili za majini

zilizopoteza maisha ya Watanzania

zaidi ya 400, serikali ya CCM

inalaumiwa kwa kushindwa

kusimamia sheria za usafiri wa majini

na kuficha taarifa ya uchunguzi wa

ajali ya awali.

Mmoja wa wabunge wa CCM ambaye

jina lake limehifadhiwa, aliilaumu

serikali kwa kuunda tume kuchunguza

ajali ya mv Bukoba na Spice Islanders,

lakini haikutoa matokeo ya uchunguzi

huo.

“Serikali iliunda tume kuchunguza ajali

ya awali ya mv Spice Islanders na mv

Bukoba lakini ikaficha matokeo ya

uchunguzi wake. Leo imetokea ajali

nyingine na binafsi naamini kama

matokeo ya uchunguzi wa awali

yangetolewa, bila shaka ajali ya juzi

ingeepukika,” alisema kada huyo.

Kufichwa kwa matokeo ya uchunguzi

wa ajali za awali za majini,

kumeelezwa kuwa ndiyo sababu ya

Spika wa Bunge, Anne Makinda,

kuzima hoja za wabunge wa kambi ya

upinzani walioungana na wabunge

wote wa Zanzibar kutaka kujadili ajali

ya mv Skagit iliyosababisha vifo vya

zaidi ya watu 150.

Chanzo: FreeMedia

Categories: