UTORO WA WABUNGE WAKWAMISHA BAJETI




•  WAPINZANI WANG’ANG’ANIA

ISIPITISHWE

na Salehe Mohamed, Dodoma

UTORO wa wabunge uliokemewa na

Spika wa Bunge, Anne Makinda, wiki

iliyopita jana ulikwamisha kupitishwa

kwa bajeti ya Wizara ya Kilimo,

Chakula na Ushirika.

Wiki iliyopita Makinda alisema utoro

kwa wabunge hivi sasa umekithiri na

akaonya kuwa kama wataendelea na

tabia hiyo ipo siku watakwamisha

upitishaji wa bajeti ya wizara husika.

Utabiri huo wa Spika Makinda, jana

ulitimia baada ya wabunge hasa wa

kambi ya upinzani kuibua hoja ya

kukwamisha upitishwaji wa bajeti ya

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika

kwa mwaka 2012/2013 kutokana na

uchache wa wabunge.

Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia

(NCCR-Mageuzi), ndiye aliyekuwa wa

kwanza kutoa hoja kwa kutumia

kanuni ya 112 ambapo alitaka bajeti

hiyo isipitishwe kwa kuwa wabunge

waliopo hawajafikia nusu ya wabunge

wote.

“Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni

inataka Bajeti ipitishwe ikiwa idadi ya

wabunge waliohudhuria itafikia nusu

ya wabunge wote.

“Hapa tulipo mimi nimeshahesabu

mara mbili wabunge wote hatuzidi

110, na tunajua idadi ya wabunge

wote ni 352 na nusu yake ni wabunge

175, ili tutende haki nakuomba

uhesabu idadi ya wabunge waliopo

kabla ya kupitisha bajeti hii ili

tuwatendee haki Watanzania,”

alisema.

Baada ya hapo alisimama Mbunge wa

Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-

Mageuzi) akitumia kanuni ya 77 (1) na

(2) kuwa wabunge waliopo hawafikii

nusu ya wabunge wote.

“Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni ya

77 (1). Akidi kwa kila kikao cha Bunge

wakati wa kufanya maamuzi itakuwa ni

nusu ya wabunge wote, kama

ilivyofafanuliwa katika ibara ya 94 ya

Katiba, isipokuwa kwamba idadi hiyo

haitahusu hoja kuhusu uamuzi wa

kubadilisha masharti yoyote ya Katiba

kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba.

“Mbunge yeyote aliyehudhuria

anaweza kumjulisha Spika kwamba,

wabunge waliopo ni pungufu ya akidi

inayohitajika kwa ajili ya shughuli

inayoendelea.

“Kwa maana hiyo, Mheshimiwa Naibu

Spika, nasisitiza kuwa hatufiki nusu

humu ndani,” alisema.

Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses

Machali (NCCR-Mageuzi) naye

alisisitiza kanuni hiyo hiyo kipengele

cha tatu. “Endapo Spika ataridhika

kwamba kweli idadi ya wabunge walio

ndani ya Ukumbi wa Bunge ni

pungufu ya akidi inayohitajika basi

atasimamisha shughuli za Bunge kwa

muda atakaoutaja na atamwagiza

katibu kupiga kengele.”

Naibu Spika Job Ndugai, alisema idadi

hiyo inatakiwa wakati wa kupiga kura

ya mwisho ya kuipitisha bajeti hiyo si

wakati wa hatua za awali za kamati ya

matumizi.

Kauli hiyo ilimfanya Mnadhimu wa

Kambi Rasmi ya Upinzani, Tundu

Lissu, asimame na kutaka kiti cha

Spika kisiliburuze Bunge kwa kukiuka

kanuni na kuliomba Bunge liahirishe

shughuli hiyo.

Hata hivyo Ndugai hakukubaliana na

kauli ya Lissu. Ndugai huku akisema

kuahirisha shughuli za Bunge ni

gharama kubwa, alichukua muda

kuamua jambo hilo.

Ndugai aliamuru Kamati ya matumizi

iendelee huku Waziri wa Nchi Ofisi ya

Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge),

William Lukuvi, alitoka nje

kuwahamasisha wabunge warejee

ukumbini. Mbali na juhudi za Waziri

Lukuvi pia kengele ilikuwa ikipigwa nje

ya ukumbi wa Bunge kuwahamasisha

warejee ukumbini.

Juhudi zakwama

Pamoja na jitihada za viongozi

mbalimbali wa serikali na Bunge

kuhakikisha idadi ya wabunge inafika

nusu, jambo hilo lilishindikana na

ndipo Ndugai alipoamua kuahirisha

shughuli za Bunge.

“Ni Vizuri wananchi waelewe kuwa

tuna huu msiba wa kitaifa

unaoendelea Zanzibar kuna wabunge

wenzetu wako kule Zanzibar hasa

kutoka Zanzibar kwa ruhusa ya

Spika…, kuna mawaziri na manaibu

wapo kule na wengine wako kule kwa

shughuli maalumu.

“Kuna wabunge kadhaa ambao mimi

mwenyewe nimewaruhusu wapo

kwenye msiba wa mazishi ya mama

wa mbunge mwenzetu, Mike Lekule

Laizer (CCM).”

Wakati Ndugai akiendelea kutoa

ufafanuzi huo, wabunge wa upinzani

walikuwa wakitoa kauli na kugonga

meza kuonesha kupinga utetezi huo.

Vitendo hivyo vilimfanya Ndugai

kuwataka wamsikilize badala ya kupiga

kelele ambazo haziwasaidii, kwakuwa

kiti cha Spika hakiwezi kumkandamiza

mtu.

“Nawaombeni ndugu zangu

tunaposikilizana kama watu wazima…

tupeane nafasi, mnalolitaka litakuwa

…..mkisema nyinyi nawapa

nafasi….mimi nikisema mnaanza

kupiga kelele.

“Inanisikitisha sana tunapovunjiana

heshima, tunakuwa kama watoto

wadogo, mimi sidhani kama

inatujengea heshima mahali popote

katika nchi yetu, tunafanya jambo la

msingi la taifa,” alisema.

Alisema kwa busara alizonazo

ameamua kuahirisha kikao hicho,

hatua ya kamati ya Bunge zima hadi

Jumatatu (kesho).

Baada ya kauli hiyo wabunge wengi

hasa wa upinzani walikuwa wakipiga

meza kwa kushangilia ‘ushindi’

walioupata.

NCCR-Mageuzi wakomalia

Mara baada ya Bunge kumalizika

wabunge wa NCCR-Mageuzi

walikutana na waandishi wa habari na

kuweka bayana kuwa hivi sasa

wanafanya uchunguzi kujua ni vikao

gani vilifanyika bila idadi ya wabunge

kutimia, baada ya hapo wapeleke hoja

kutaka maamuzi yaliyofikiwa

yatenguliwe.

Mbunge wa Kasulu Kusini, David

Kafulila, alisema maamuzi mengi

yamekuwa yakifanywa bila akidi

kutimia, jambo ambalo ni hatari kwa

maendeleo ya taifa.

“Tutaomba Spika atupe orodha ya

wabunge waliohudhuria katika kikao

hiki cha Bajeti na tukibaini tutaomba

maamuzi yaliyoafikiwa yatenguliwe,”

alisema.

Chanzo FreeMedia

Categories: