Showing posts with label Mkuu wa Mkoa. Show all posts
Showing posts with label Mkuu wa Mkoa. Show all posts

MKUU WA MKOA ARUSHA AAMURU MTENDAJI NA MFANYA BIASHARA WA SUKARI WAKAMATWE KWA ULANGUZI


Na Gladness Mushi- Arusha

Mkuu wa mkoa wa Arusha ambaye kwa sasa ndiye anayeshikilia wadhifa huo Bw Magesa Mulongo amesema kuwa kamwe hatakubali kuona mkoa wa arusha ukiwa unaangamia kwa ajili yabaadhi ya viongozi ambao si wazalendo wa nchi
Bw Magesa aliyasema hayo mapema leo wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa mji wa arusha kwa mara ya kwanza mara baada ya kuchaguliwa kwake.
alisema kuwa ili kiongoiz kama kiongozi aweze kuitwa kiongozi ni lazima kwanza avae kofia ya uongozi na walasio kofia ya uchu wa madaraka kwa kuwa hali hiyo inafanya kazi nyingi kushindwa kufanyika kwa wakati huku wananchi wakiendelea kuumia.
Aliongeza kuwa hali hiyo kwa sasa ndani ya mji wa arusha itakwaisha kabisa kwa kuwa hata penda kwenda kufanya kazi aliyopewa na baadhi ya viongozi majina kwa kuwa mji wa arusha bado unakabiliwa na mambo mengi sana
Alisema kuwa kwa kiongozi ambaye hataweza kufanya kazi pamoja nay eye ni bora achie ngazi kwa kuwa viongozi wazembe ndio wanaochangia kwa kiwango kikubwa sana kuongezeka kwa changamoto nyingi ndani ya jamii ya watanzania
“leo mpo hapa wote napenda kuwaambia kuwa kamwe mimi sitaenda kwenye uongozi na mtu ambaye anajua anachokifanya kuwa ni kibaya na kwa hali hiyo leo nawatangazia wazi kuwa anayejijua kuwa anatabia ya kuwa moto baridi ni bora achie madaraka”alisema bw Magesa
Katika hatua nyingine aliwataka wakuu wa idara kuhakikisha kuwa wanafuatilia mambo mbalimbali ambayo yanafanyika kama vile miradi ndani ya miji na kata kwa kuwa baadhi ya wakuu wa idara ndio chanzo cha uharibifu wa kazi za jamii
Bw Magesa alisistiza kuwa hali ya kukaa tu ofisini kwa baadhi ya watendaji inafanya shuguli mbalimbali za kijamii kufanikishwa chini ubora wa viwango na watendaji wabovu kwa kuwa wanajua hawawezi kukaguliwa.
“leo unakuta mtendaji eti amekaa ofisini anapitisha malipo kwa mkandarasi sasa huyu mkandarasi jue kama amejenga chini ya ubora utajuaje lakini kama utakuwa unafuatlia na kukagua ujenzi na miradi mbalimbali hasara hazitatokea tena ndani ya miradi yetu”alieleza bw Magesa
Pia aliwataka madiwani wa jiji kuhakikisha kuwa wanaweka utaratibu wa kujua takwimu za miradi mbalimbali ambayo imo kwenye kata zao kwa kuwa nao baadhi ya madiwani hawana takwimu sahihi juu ya miradi
Mkuu huyo alisema kuwa madiwani wanatakiwa kujua na kutambua kuwa wanaiwakilisha serikali ikiwa ni pamoja na wananchi ambao waliwaamini na kuwapa kura kwa hali hiyo basiwanatakiwa kuhakikisha kuwa wanafanya kazi sana bila kujali itikadi zao
Alimalizia kwa kusema kuwa endapo kama watafanya hivyo ni wazi kuwa jiji litakuwa na maendeleo mengi kwa kuwa mji wa arusha ndio kivutio pekee cha mji wa Tanzania.

[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MKUU WA MKOA WA MOROGORO ATEMBELEA MGODI WA KUZALISHA UMEME WA BWAWA LA KIHANSI


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( aliyekaa kwenye kiti) akioneshwa sehemu inayokontroo masuala mbalimbali ya umeme baada ya kuvuliwa na kuingia kwenye gridi ya taifa kutoka mgodi wa kuzalisha umeme wa Bwawa la Kihansi, kutoka kwa Msimamizi mwandamizi wa uwezeshaji na usimamizi wa mfumo wa kompyuta , Christopher Mahundi (mwenye rula ) juu ya usimamizi wa matukio mbalimbali ndani ya mgodi huo Oktoba 14, mwaka huu.Picha na John Nditi.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»

MKUU WA MKOA WA RUKWA AIOMBA OFISI YA MWANASHERIA MKUU KUISAIDIA TAKUKURU


Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akizungumzia mambo muhimu ya kisheria na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Eng. Stella Manyanya (MB) ofisini kwake leo asubuhi. Miongoni mwa mambo aliyoyasisitiza ni haki iwe inapatikana kwa wote na kwa wakati pamoja na suala zima la uzalendo kwa watendaji wote wa Serikali na mahakama.


Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ofisini kwake.

****

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Eng. Stella Manyanya (MB) ameiomba ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia kwa Naibu Mwanasheria Mkuu Mhe. George Masaju kuisaidia Tume ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kuweza kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi ya ilivyo hivi sasa.

Alimueleza hayo alipomtembelea ofisini kwake leo asubuhi ambapo atakuwa na Ziara ya siku mbili kutembelea Idara ya Mahakama, Jeshi la Magereza, Polisi na TAKUKURU.
Alimueleza kuwa TAKUKURU inatakiwa kiwe chombo makini kinachofanya mambo kwa usahihi na kwa kutoa mamaamuzi mazito na yenye uhakika zaidi.

Alimueleza kuwa elimu ikitumika vizuri ni muhimu kuweza kuepusha migogoro na matatizo ya Rushwa na haki za kibinadamu nchini. Kwa upande wake Naibu Mwanasheri Mkuu wa Serikali alikiri na kusema kuwa nilishawaeleza TAKUKURU kuwa kwenye upande wa uelimishaji wa Umma juu ya athari na matukio ya Rushwa hawajaufanya vizuri.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alimuahidi Naibu Mwanasheria Mkuu huyo kutumia ziara zake mkoani kuelimisha wananchi juu ya madhara ya rushwa, utambuzi wa haki zao za msingi, uzalendo na udumishaji wa amani ambayo ndio ngao kuu watanzania waliyojijengea kwa miaka mingi iliyopita.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju yupo Mkoani Rukwa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili akitokea Songea ambapo atatembelea Idara ya Mahakama, Jeshi la Polisi, Magereza na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Ziara hiyo inahusu "Nationa Criminal Justice Forum" inayolenga katika kuzungumzia na kutatua matatizo yanayopatikana katika Idara ya Mahakama, Jeshi la Polisi, Magereza na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa.

Kwa mujibu wa Naibu Mwanasheria Mkuu huyo wa Serikali alisema kuwa katika ziara yake hiyo na kwa maeneo anayotembelea wanaweka mkazo zaidi kwenye mambo matatu muhimu ambayo ni ubora wa huduma zinazotolewa, Utambuzi na utayari katika kusimamia haki (Sensitivity to Justice) na kutilia mkazo kwenye Uzalendo katika utekelezaji wa shughuli za Serikali.
[ Read More ]

Posted by newstz.blogspot.com 0 comments»