LOWASSA ACHANGISHA MIL 126.9 ZA UJENZI WA MABWENI SEKONDARI YA ASKOFU JOHN SEPEKU ILIYOPO BUZA MTONI, DAR ES SALAAM



Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikani Tanzania, Valentino Mokiwa (kushoto) akipokea mchango wa sh. mil 10 kutoka kwa mke wa Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa (katikati), Regina Lowassa, zilizotolewa na familia ya Lowassa katika harambee ya kuchangia fedha za ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari ya Askofu John Sepeku iliyopo Buza Mtoni, Dar es Salaam. Lowassa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo iliyofanyika Kanisa la Aglikani Segerea, Dar es Salaam leo, ambapo zaidi ya sh. mil. 126.9 zilichangangwa. Waziri Mkuu mstaafu aliahidi kutoa tena sh. milioni 10. 

Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikani Tanzania, Valentino Mokiwa (kushoto), akimshukuru Mbunge wa Jimbo la Segerea, Dk. Makongoro Mahanga ambaye alichangia sh. mil. 3,katika harambee ya kuchangia fedha za ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari ya Askofu John Sepeku iliyopo Buza Mtoni, Dar es Salaam.
Mtoto David Gideon (4), akitoa mchango wake wa sh. 1000 kwa Askofu Mkuu Valentino Mokiwa kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa mabweni ya shule hiyo.


Mke wa Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa (kulia) akikumbatiana kwa furaha na mke wa Askofu Mokiwa, Mama Grace Mokiwa,  wakati wa harambee hiyo.

Baadhi ya waumini wakishangilia baada ya Waziri Mkuu mstaafu, Eward Lowassa kutangaza kuvuka kwa malengo ya harambee hiyo, ambapo malengo yalikuwa kukusanya sh. mil. 100 lakini zilichangwa sh. mil 126.9.
Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa (kulia) akisalimiana na baadhi ya waumini wa Kanisa la Anglikani, waliochangia fedha katika harambee hiyo.

Categories: