MAZISHI YA MABAKI YA MIILI YA ABIRIA WA DELUX



Shughuli ya ya kuzika mabaki ya miili ya abiria waliopata ajali walipokuwa wakisafiri kutoka Dar es salaam kuelekea Dodoma juzi. Ajali hiyo ilitokea Kibaha, mkoa wa Pwani, baada ya gurudumu la mbele la basi la Delux kupasuka na kusababisha kudondoka na kuwaka moto na kuteketea kabisa pamoja na abiria 12 hapo hapo. Mazishi hayo ya pamoja yamefanyika katika makaburi ya eneo liitwalo Air Msaehapo Kibaha ambako mwaka 1999 ajali ingine ilitokea sehemu hiyo hiyo. Marehemu imebidi wazikwe pamoja baada ya miili yao kuungua vibaya sana kiashi cha kushindwa kutambulika.

Picha na Chris Mfinanga

Categories: ,