Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»
Showing posts with label Pinda. Show all posts
Showing posts with label Pinda. Show all posts
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama tembo wakati aliposimama kwa muda kwenye Lodge ya Katuma Bush katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi wilayani Mpanda wakati alipoitembelea kukagua athari za kiangazi kwenye Hifadhi hiyo Oktoba 20,2011.
Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»
Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri mkuu Mizengo Pinda wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wawekezaji na mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi hapa nchini muda mfupi baada ya Rais Kikwete kufungua kongamano la uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanganyika huko Mpanda mkoani Rukwa lao mchana.
(picha na Freddy Maro).
Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua madini yanayochimbwa Mpanda wakati alipotembelea banda la TPM MINING COMPANY LIMITED katika maonyesho yatakayoambatana na uzinduzi wa mkutano wa uwekezaji unaotarajiwa kufunhuliwa na Rais Jakaya Kikwete Mjini Mpanda October 17,2011.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Rais wa zamani wa Brazil,Luiz Lula baada ya mazungumzo yao kwenye hoteli ya Marriott katika mji wa Des Moines, Iowa,Marekani October 13, 2011. Baadae Rais huyo alitunukiwa nishani ya Food Prize.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Rais wa World Food Prize, Balozi Kenneth Quinn wakifurahia baada ya Waziri Mkuu kutoa salamu za Rais Jakaya Kikwete kwenye Mkutano wa World Food Prize kwenye hoteli Marriott aktika mji wa Des Moines, Iowa, Marekani October 13,2011.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»
Imeandikwa na Joseph Kulangwa, Sao Paulo
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amekunwa na teknolojia ya kilimo cha muhogo, ambapo mashine maalumu zinatumika kupandia zao hilo tofauti na Tanzania ambako kilimo hicho bado ni cha kiwango cha chini na duni.
Waziri Mkuu alioneshwa kukunwa na teknolojia hiyo juzi alipotembelea kampuni ya kutengeneza vifaa na mashine za kilimo ya ABIMAC mjini hapa akiwa katika ziara yake ya kikazi nchini Brazil.
Hata hivyo, alisema maendeleo hayawezi kupatikana bila kufanya kazi kwa bidii, lakini pia kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Alilazimika kusema hayo alipopewa fursa ya kufanya hivyo baada ya kuangalia video ya mambo yanayofanywa na kampuni hiyo yenye matawi katika mikoa 10 nchini hapa na kampuni tanzu 4,500.
Waziri Mkuu alisema kwa Tanzania teknolojia hiyo inapaswa kutekelezwa hatua kwa hatua na si kuikimbilia.
Akizungumzia juu ya teknolojia ya kilimo cha muhogo, Pinda alisema: “Tunaweza kutumia fursa hii kuboresha kilimo cha muhogo ... tunaweza kuula, lakini ni vema sasa nasi tukaanza kuuza nje pia,” alishauri.
Kuhusu mifugo, alisema teknolojia ya kutengeneza chakula cha mifugo kutokana na majani ya kawaida, miwa na mahindi, inaweza kuwasaidia wafugaji nchini Tanzania.
“Sisi kwetu Tanzania tuna mifugo takribani milioni 21, lakini Afrika kwa jumla tuna tatizo ... hali ya hewa inapobadilika tu mifugo hukosa chakula na kufa, lakini kwa teknolojia hii tunaweza kuiokoa,” alisema.
Naye Waziri wa Ardhi na Maji Zanzibar, Ali Juma Shamuhuna ambaye anafuatana na Waziri Mkuu, alieleza kuvutiwa na teknolojia hiyo ya kilimo cha muhogo na chakula cha mifugo, akisema inaweza kuwasaidia Watanzania kama wataamua kuitumia kikamilifu.
Alisema teknolojia hiyo inaweza kusaidia wakulima na wafugaji kuinua hali yao ya kipato na hata kuondokana na umasikini lakini ikitumiwa vizuri.
Mbunge wa Rufiji, Dk. Seif Rashid alisema teknolojia hiyo inawezekana ingawa ni mpya, lakini akasema Watanzania wanaweza kufundishwa wakaielewa na kuitumia kujiendeleza.
Baadaye ujumbe wa Pinda ulitembelea kiwanda cha kutengeneza nishati ya ethanol itokanayo na miwa inayozalishwa na Kampuni ya Construtora Queiroz Calvao S/A.
Akiwa hapo hapo wilayani Piracicaba, Waziri Mkuu na ujumbe wake walitembelea kampuni nyingine ya Dedini ambayo licha ya kutengeneza mitambo ya kuzalishia ethanol inayotengeneza pia bidhaa mbalimbali za kiteknolojia pamoja na chakula na vinywaji.
Chanzo: Habari leo
[ Read More ]
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amekunwa na teknolojia ya kilimo cha muhogo, ambapo mashine maalumu zinatumika kupandia zao hilo tofauti na Tanzania ambako kilimo hicho bado ni cha kiwango cha chini na duni.
Waziri Mkuu alioneshwa kukunwa na teknolojia hiyo juzi alipotembelea kampuni ya kutengeneza vifaa na mashine za kilimo ya ABIMAC mjini hapa akiwa katika ziara yake ya kikazi nchini Brazil.
Hata hivyo, alisema maendeleo hayawezi kupatikana bila kufanya kazi kwa bidii, lakini pia kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Alilazimika kusema hayo alipopewa fursa ya kufanya hivyo baada ya kuangalia video ya mambo yanayofanywa na kampuni hiyo yenye matawi katika mikoa 10 nchini hapa na kampuni tanzu 4,500.
Waziri Mkuu alisema kwa Tanzania teknolojia hiyo inapaswa kutekelezwa hatua kwa hatua na si kuikimbilia.
Akizungumzia juu ya teknolojia ya kilimo cha muhogo, Pinda alisema: “Tunaweza kutumia fursa hii kuboresha kilimo cha muhogo ... tunaweza kuula, lakini ni vema sasa nasi tukaanza kuuza nje pia,” alishauri.
Kuhusu mifugo, alisema teknolojia ya kutengeneza chakula cha mifugo kutokana na majani ya kawaida, miwa na mahindi, inaweza kuwasaidia wafugaji nchini Tanzania.
“Sisi kwetu Tanzania tuna mifugo takribani milioni 21, lakini Afrika kwa jumla tuna tatizo ... hali ya hewa inapobadilika tu mifugo hukosa chakula na kufa, lakini kwa teknolojia hii tunaweza kuiokoa,” alisema.
Naye Waziri wa Ardhi na Maji Zanzibar, Ali Juma Shamuhuna ambaye anafuatana na Waziri Mkuu, alieleza kuvutiwa na teknolojia hiyo ya kilimo cha muhogo na chakula cha mifugo, akisema inaweza kuwasaidia Watanzania kama wataamua kuitumia kikamilifu.
Alisema teknolojia hiyo inaweza kusaidia wakulima na wafugaji kuinua hali yao ya kipato na hata kuondokana na umasikini lakini ikitumiwa vizuri.
Mbunge wa Rufiji, Dk. Seif Rashid alisema teknolojia hiyo inawezekana ingawa ni mpya, lakini akasema Watanzania wanaweza kufundishwa wakaielewa na kuitumia kujiendeleza.
Baadaye ujumbe wa Pinda ulitembelea kiwanda cha kutengeneza nishati ya ethanol itokanayo na miwa inayozalishwa na Kampuni ya Construtora Queiroz Calvao S/A.
Akiwa hapo hapo wilayani Piracicaba, Waziri Mkuu na ujumbe wake walitembelea kampuni nyingine ya Dedini ambayo licha ya kutengeneza mitambo ya kuzalishia ethanol inayotengeneza pia bidhaa mbalimbali za kiteknolojia pamoja na chakula na vinywaji.
Chanzo: Habari leo
Posted by newstz.blogspot.com
0
comments»